BUNGE LAAHIRISHWA LEO HUKU HOJA YA MGOMO WA MADAKTARI IKIIBUKA KWA MARA YA SITA BUNGENI,SPIKA KUTOA UFAFANUZI KESHO.
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa wamesimama mara baada ya Naibu Spika wa Bunge Job Ndugay Kuahirisha kikao cha Bunge leo mjini Dodoma.Pamoja na mambo mengine yaliyojitokeza wakati wa kuahirisha kikao hicho ni hoja ya Mgomo wa madaktari ambayo iliibuliwa na mbunge wa Kigoma mjini Peter Selukamba ambaye aliitaka serikali kutoa tamko la hatma ya mgomo huo ambapo Naibu spika Job Ndugay aliwataka wabunge kuwa na subira ili Ofisi ya spika ikutane na kamati ya uongozi ya bunge ili kutoa maamuzi hapo kesho kabla ya kuahirisha mkutano huo wa sita.
Aliyekuwa waziri mkuu na mbunge wa Monduli Edward Lowasa (kushoto) akijadili jambo na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu Stephen Wasira (katikati) na mbunge wa viti maalum CHADEMA Leticia Nyerere leo mjini Dodoma.
Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dkt. Terezya Huvisa (Kulia) akizungumza na Zainabu Kawawa mbunge wa viti maalum CCM mara baada ya kumalizika kwa kikao cha saba cha bunge leo mjini Dodoma.
Comments