WANACHAMA WA VICOBA KATA YA KIWERE WAMPONGEZA MBUNGE WA JIMBO LA KALENGA KWA KUWAONGEZEA NGUVU


Mbunge  wa  jimbo la Kalenga  Godfrey Mgimwa kushoto akipongezwa na mmoja kati ya  wapiga kura wa kijiji cha Kiwere
Mfanyabiashara  wa  nyama  choma Kiwere  kulia akimweleza  mbunge  Mgimwa  jambo baada ya kutembelea  vijana  na  wananchi  wanaojishughulisha na biashara eneo la magenge ya Kiwere 
wanakikundi  cha uoteshaji  miti Kiwere wakimweleza  mikakati yao mbunge Mgimwa katikati 
Mbunge wa  jimbo la Kalenga  Godfrey Mgimwa akipita kwa shida katika  vichaka baada ya kwenda  kuwatembelea  wapiga kura  wake  kijiji  cha Kiwere 
Kama  anazungumza   vile "lazima nimefike  kuona kazi za  wapiga kura  wangu "
Mbunge wa Kalenga Bw Mgimwa katikati  akiruka maji  ili kwenda  kuona mto  ambao unatumika kuwapa huduma ya maji wakazi wa Kiwere 
Wanachama wa VICOBA Kiwere  wakiimba shairi  mbele ya mbunge Mgimwa 
Diwani wa kata ya Kiwere  Pachal Mwano  akizungumza kabla ya  kumpongeza  mbunge  Mgimwa kwa kazi nzuri 
Mbunge Mgimwa akizungumza na  wanachama wa Vicoba Kiwere 
Wanachama  wa  Vicoba  Kiwere  wakifuatilia  hotuba ya  mbunge  Mgimwa

Na  Matukiodaima.co.tz
WANACHAMA  wa  vikundi  vya  VICOBA  kata ya  Kiwele  katika jimbo la Kalenga  mkoani Iringa  wapongeza jitihada za  mbunge  wao Godfrey Mgimwa  kwa  kuwachangia  kiasi cha Tsh milioni 3  ili  kukuza mfuko  wa vikundi  hivyo  kata ya Kiwele.

Akitoa  pongezi  hizo jana  kwa niaba ya  wanachama  wa  VICOBA  kata ya  Kiwele diwani  wa kata  hiyo Paschal Mwano  alisema  kuwa  kata  hiyo ni  miongoni mwa kata  zenye ndoto  kubwa ya  kuanzisha  benki ya  wananchi wa kata ya Kiwele  hivyo  kutokana na jitihada mbali mbali mbali  zinazofanywa na  wananchi hao kwa kuungana katika  vikundi hivyo ipo siku  watafikia hatua ya kuwa na benki 

Kwani  alisema  kuwa  fedha  hizo  kiasi cha  Tsh  milioni 3  zilizotolewa na mbunge  huyo  zitasaidia  kukuza  mtaji wa  vikundi  hivyo   22 zilivyopo katika kata  hiyo  yenye  vijiji  vitano kikiwemo cha Kiwere , Mgera, Mfyome ,kitapilimwa na Itagutwa .

Alisema  kuwa vikundi  hivyo   hivyo  vina  jumla ya  wanachama  464 wakiwemo  wanawake  386 na wanaume 78 na  hadi  sasa  wana jumla ya Tsh 33835000  na  kuwa  kutokana na na  faida  mbali mbali  wanazozipata  katika  vikundi  hivyo  wanachama wameweza  kuanzisha  miradi mbali mbali  ikiwemo ya ufugaji kuku ,bata  nyuki  na  miradi mingine mingi ambayo imewasaidia kukuza  uchumi wa mwanachama mmoja mmoja.

Mbali ya kujiwezesha  kwa  mikopo  bado wanahitaji  kusaidiwa mitaji  zaidi  ili  kuanzisha miradi ya  ufugaji ng'ombe wa maziwa na kuku wa nyama na mayai   kama  njia ya  kuongeza  miradi  zaidi.

Kwa upande  wake  mbunge  Mgimwa pamoja na  kuwapongeza kwa  kuanzisha  vikundi  hivyo 22 vya  vicoba  bado  alisema  kuwa  kasi kubwa ya  wananchi  kuendelea  kujiunga  na  vikundi  hivyo  vya Vicoba  ndio itakayopelekea  jimbo la Kalenga  kuja  kuwa na benki ya  wananchi wa Kalenga jambo ambalo linawezekana.

" Nawapongeza  sana  wananchi  wa kata ya  Kiwere  kwa  kuendelea  kujiunga na Vicoba kwani naamini  njia  pekee ya kujikomboa kiuchumi ni pamoja na  hii ya  kujiunga pamoja  ......kwa  hatua  ambayo  mmefikia   tunaweza  kufanya  jambo  kubwa  zaidi ya  hili mimi  leo  nitawachangia  kiasi cha Tsh milioni 3  ili  kukuza mtaji  zaidi " alisema  mbunge Mgimwa 

Aidha  alisema  kuwa  tatizo  kubwa katika vikundi  hivyo  vya kifedha ni pale ambapo  wanachama  wanakopa na  kushindwa  kurejesha mikopo kwa  wakati na  hivyo  kukwamisha wanachama  wengine  kukopa .

Kuwa  iwapo  wanachama  watashindwa  kurejesha  mikopo  kikundi ama  vikundi  hivyo havitaendelea  na badala  yake  vitakufa mapema hivyo  kuwataka  wakopaji  kulipa mikopo kwa  wakati kama njia ya  kuviendeleza  vikundi  hivyo.

Mbunge  Mgimwa  alisema  kuwa kitaalum  yenye ni mtaalam wa    fedha  hivyo kwa  kupitia  uwezo  wake  ndio  sababu ya bunge  kumteua  kuwa mjumbe wa kamati ya bunge ya  bajeti ya  serikali na wana kalenga  wazidi  kujivunia kumpata  mbunge  mwenye  ndoto ya  kuona  jimbo  hilo linakuwa na benki ya  wananchi wa Kalenga  jambo ambalo  linawezekana kufanyika.

Kawaida

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*