Elimu ya awali Tunduru na changamoto zake

Mwalimu wa darasa la awali wa Shule ya Msingi Nakayaya, Teckla Milanzi (kulia) akiwa na wanafunzi wake eneo ambalo hutumika kama darasa la wanafunzi hao.
Mwalimu wa darasa la awali wa Shule ya Msingi Nakayaya, Teckla Milanzi (kulia) akiwa na wanafunzi wake eneo ambalo hutumika kama darasa la wanafunzi hao.
WADAU wa elimu nchini Tanzania wanaamini kwa kiasi kikubwa kwamba endapo elimu ya awali (chekechea) nchini Tanzania itatolewa katika misingi inayostahiki itakuwa ni njia moja wapo madhubuti ya kuimarisha ubora wa elimu. Hii ndiyo maana wanaendelea kupaza sauti wakiitaka serikali kupitia vyombo husika kuboresha kwanza elimu ya awali kabla ya kupanda ngazi nyingine za juu.
Huenda kilio hiki cha wadau wa elimu kimeanza kusikika serikalini. Kwani tayari Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi iliagiza tangu mwaka 2010 kuwa kila shule zake za msingi ni lazima lianzishwe darasa la awali ili kuwenza kuwaandaa wanafunzi kuingia na darasa la kwanza. Awali elimu hii ilikuwa ikitolewa kwa kiasi kikubwa na taasisi na vikundi mbalimbali na hata watu binafsi nje ya shule za msingi, tena kwa hiyari. Kwa sasa sera na miongozo ya elimu inatamka wazi kuwa nilazima kila shule ya msingi iwe na darasa la awali kwa ajili ya elimu hiyo muhimu.
Changamoto kubwa iliyoibuka kwa sasa baada ya utekelezaji wa agizo hilo ni namna elimu hiyo inavyoendeshwa kwa kusuasua kwenye baadhi ya shule za Serikali. Hivi karibuni mwandishi wa makala haya alitembelea baadhi ya shule za msingi zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kuangalia hali ya utekelezaji wa zoezi hilo.
Uchunguzi ulibaini zipo shule ambazo licha ya kusajili wanafunzi wa awali kila mwaka hazina madarasa ya kusomea kwa watoto hao, hali ambayo inafanya wanafunzi hao wadogo kufundishwa katika mazingira magumu na kudhohofisha lengo zima la utoaji wa elimu hiyo. Wapo wanafunzi ambao hulazimika kufundishiwa nje, yaani chini ya mti ama kwenye magofu (majengo ya shule ambayo hayajakamilika) iwe madarasa au nyumba za walimu.
Teckla Milanzi ni mwalimu wa darasa la awali, Shule ya Msingi Nakayaya. Anasema kimsingi wanafunzi wa darasa la awali shuleni hapo wanasomea chini ya mti kwa kuwa hawana darasa maalum kwa wanafunzi hao. Anasema wakati wa mvua ama jua kali mara nyingine hulazimika kuhairisha masomo kwa siku kutokana na hali ya hewa.
Baadhi ya wanafunzi wa darasa la awali katika Shule ya Msingi Tunduru Mchanganyiko wakiwa darasani kama walivykutwa na mwandishi wa makala haya hivi karibuni.
Baadhi ya wanafunzi wa darasa la awali katika Shule ya Msingi Tunduru Mchanganyiko wakiwa darasani kama walivykutwa na mwandishi wa makala haya hivi karibuni.
Anasema anashukuru kwa sasa wanajihifadhi kwenye jengo moja ambalo linaendelea na ujenzi shuleni hapo, jengo ambalo hata hivyo mara baada ya ujenzi kukamilika na wahusika kukabidhiwa darasa watarudi kusomea chini ya mti kama ilivyo ada. Hata hivyo, anasema licha ya changamoto hiyo darasa hilo halina vitabu kwa ajili ya kufundishia wanafunzi, bali kuna nakala moja moja kwa baadhi ya masomo ambavyo vilitafutwa kwa jitihada za mwalimu mwenyewe.
“Mfano kwa vitabu vya Kiswahili, Kiingereza, Sayansi na Hisabati kuna nakala moja moja tu, ambazo hutumiwa na mwalimu mwenyewe. Anasema darasa hilo licha ya kuwa na changamoto kedekede hata kwenye mgao wa fedha zinazoletwa shuleni kila mara halimo hivyo hakuna kinacholetwa tofauti na wanafunzi wengine,” anasema Bi. Teckla Milanzi.
Kwa upande wake, Mwalimu Christina Komba wa darasa la awali Shule ya Msingi Tunduru Mchanganyiko anasema madarasa ya elimu ya awali Wilayani Tunduru yanakabiliwa na changamoto nyingi. Anabainisha kuwa madarasa mengi likiwemo lake hawana vitabu wala miongozo ya namna ya ufundishaji kabisa zaidi ya kila mwalimu anayefundisha kubuni nini afundishe kila uchao.
“…Kwanza licha ya kutokuwa na vifaa vingine hatuna chumba maalumu cha wanafunzi hawa (darasa) kwa sasa tunatumia jengo la darasa ambalo bado linaendelea na ujenzi na hata hivyo jengo hili halijengwi kwa ajili ya wanafunzi wa awali,” anasema mwalimu Christina Komba.
Wanafunzi wa darasa la awali katika Shule ya Msingi Nakayaya, wakiwa katika darasa lao.
Wanafunzi wa darasa la awali katika Shule ya Msingi Nakayaya, wakiwa katika darasa lao.
“Madarasa ya elimu ya awali hayana vitabu, hayana miongozo…huwa tunaanzima au ukipata hela yako wewe binafsi unaenda kununua kitabu kimoja au viwili ili uweze kuwasaidia watoto. Na baadhi ya masomo hayana vitabu kabisa hata ukienda madukani katika Wilaya yetu (Wilaya ya Tunduru) vitabu kama Haiba na Michezo, pamoja na Sanaa hazipo kabisa madukani. Anasema uongozi wa juu wilayani unalitambua hilo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA