JAMII YA KIKURUDI WAKE KWA WAUME WATOTO WAZEE WASHIKA SILAHA KUULINDA MJI WAO KOBANE DHIDI YA WAPIGANAJI WA ISLAMIC STATE WASIUTEKE MJI WAO


 UMOJA NI NGUVU_Mwanamke wa Kikurudi na mwanae akiwa na bunduki aina ya AK-47 Tayari kuwakabili wapigaji wa Dola ya kiislam wasiuteke mji wao kobane asubuhi ya leo
 Jengo la gorofa likionekana kileleni bendera ya kundi la Isis ikipepea,katika mji wa kobane,tukio hili limefanya kobane nzima kutaharuki.
 Moshi mkubwa angani hii ni baada ya mashambulizi ya anga yakilenga sehemu ambazo inasemekana wapigaji wa Isis wamejificha.
 UTURUKI_Waturuki wakijipiga picha mpakani kama kumbukumbu ,nyuma yao unaonekana moshi ukipaa angani baada ya ndege za kivita za marekani kufanya mashambulizi ya Anga.
 Wana_nchi wakituruki wanaoishi mpakani na Syiria,wamekuwa wajijitokeza kwa wingi kushuhudia mapigano yanavyoendelea hasa jinsi jamii ja wakurudi walivyojitokeza wote bila kujari jinsia umri nakubeba siraha kuulinda mji wao usitekwe na Isis.
 Wa_Turuki wakiangalia kwa mbali mapgano na hasa ndege za marekani zinavyofanya mashambulizi ya anga.
 Mturuki akipiga picha kwa mbaali
 Mpiganaji wa Dola ya Ki_islaam akiwa na siraha yake mkononi,alikuwa akiongea kwamba mafaniko yao yanatokana na uwezo waliopewa na Alah,na kwamba hakuna wakuwazuia kuuteka mji wa kobane muda si_mrefu,na kuwateketeza makafiri wote.
 Wapiganaji wa ISIS wakiwa juu ya miinuko katika harakati zao za kuuteka mji wa kobane
Waturuki wakiangalia kwa mbaali mapigano kati ya kabira la wakurudi dhidi ya Isisasubuhi ya leo.
 
Habari kwa hisani ya mtandao wa Daiyl mail.
 
 
SYRIA-Licha ya mashambulizi makubwa yanayofanywa na jeshi la anga la Marekani na washirika wake  dhidi ya wapiganaji wa Dola ya ki-islaam isis,rakini wapiganaji hao wameweza kusonga mbele nakuukabili mji uliopo  mpakani,wako juu ya viunga na milima wakiuangalia kobane kwa chini,
Kobane ni Syria mji unaopakana na Uturuki ambao wakazi wake ni jamii ya Kikurudi ,kabila linalojiona limebaguliwa huko katika nchi ya Uturuki na mala nyingi wamekuwa wakitaka kutambuliwa kama Taifa huru bila mafanikio,ni kabila lililopo katika nchi za  Uturuki, Iraqi  na Syiria.
Mapigano ya leo asubuhi kati ya wanajeshi wa kikurudi wakisaidiwa na Marekani zidi ya Isis imeleta taharuki kubwa kwa jamii nzima inayoishi katika huo mji wa kobane,na wanaonakuna hatari mji wao wakati wowote kutekwa,na kuangukia mikononi mwa isis ,hii inatokana na kusonga mbele katika uwanja wa mapambano,  kwa wapiganaji hao na wamefanikiwa kuteka milima na viunga vinavyoikabili kobane,na wapiganaji hao wameapa kuuteka huo mji na kuharibu na kuwaangamiza makafiri wote katika mji huo wa Syria unaopakana na nchi ya uturuki,hali hiyo imewafanya wakurudi wote bila kujali mtoto au mwanamke wameungana nakushika sira za aina mbalimbali za kisasazikiwemo AK_47 kuulinda mji wao usiangukie mikononi mwa magaidi isis,nae msemaji wa wapiganaji wawakurudi ,ameonya jamii ya kimataifa kwamba iwapo isis itafanikiwa kuuteka mji wa kobane basi yanaweza kutokea mauaji ya kimbari,na kwamba inatakiwa mikakati kuweza kuwazuia isis wasiuteke huo mjiitakuwa vigumu kwa wapigaji wa _kikurudi kuwazuia na kuwalinda wananchi wake iwapo Isis itafanikiwa yatatokea maafa makubwa,
Nae shuhuda aliyepo katika uwanja wa mapambano amesema kundi la isis baada ya kuona linapata upinzani kutoka mashambulizi ya anga,limebuni mbinu ya kutokwenda katika makundi makubwa kitu kinachofanya kuonekna na majeshi ya Marekani nakushambuliwa kwa urahisi wamejiunda  katika makundi madogo madogo kitu kinachofanya Marekani kutokujua hasa wapi walipo,pia isis wapiganaji wake wamekuwa wanaenda sambamba na vifaru vyao katika harakati zao za kusonga mbele,
Wakati yote hayo yakitokea uturuki imesogeza majeshi yake mpakani bila kutoa msaada wowote ule,na wananchi wake wamejitokeza kwa wingi mipakani huku ikiangalia tu , jinsi wapiganaji wa kikurudi wake kwa wa ume watoto wazee walivyojiunga pamoja kuulinda mji wao kobane usitekwe ,imekuwa ni sinema ya bure kuangalia kinachotokea alisikika mturuki mmoja aliyekuwa na wenzake wakipiga picha upande wa pili ,huku ndege za Uingereza na Marekani zikiendelea kufanya mashambulizi ya anga sehemu ambazo wanahisi wapo wapinaji wa Isis.
Waziri mkuu wa Uturuki amesema na kuonya kwamba mashambulizi ya anga yanayofanywa na ndege za marekani ,hazijasaidia chochote kile na msaada wake ni mdogo na nikama vile umechelewa wapiganaji wa kikurudi wanaosaidiwa na marekani ni kama vile wamezidiwa nguvu na wapiganaj,i wa dola ya kiislaam alisema waziri mkuu wa uturuki,yanahitajika majeshi ya ardhini yaingilie kati upesi iwezekanavyo.
Bendera za isis zimekuwa zikionekana zikipepea katka majengo marefu ya kobane na viunga vyake kuashiria kwamba wakati wowote mji utakuwa chini ya wapiganaji hao,Nao wapiganaji wa dola ya kiislamu katika mkanda wao waliourusha hivi punde wamesikika wakisema na kujigamba kwamba mafanikio yao waliyoyapata yanatokana na Alah kuwa upande wao ,pamoja nakushambuliwa kutoka angani na majeshi ya Marekani na washirika wao rakini Mungu wao Alah ananguvu kuliko Marekani na wameahidi kuuteka kobane na kuwaangamiza makafiri wote alisema msemaji wao aliyekuwa amebeba silaha.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.