WANAFUNZI DARASA LA SABA SHULE YA ADOLPH KOPING BUKOBA WATEMBELEA KIWANDA CHA SUKARI KAGERA.

Wanafunzi wa Darasa la Saba (Adolph Kolping English Medium Primary School) wametembelea kiwanda cha Kagera Sugar kilichopo Bukoba na kujionea utengenezaji wa Sukari ikiwa ni sehemu ya mafunzo yao.

Kiwanda cha Sukari cha Kagera tayari kilishaanza kuzalisha ziada ya sukari inayohitajika katika soko la sukari Nchini hali inayopelekea kuweza kupunguza tatizo la upatikanaji wa sukari Tanzania na Nchi za jirani zinazotumia sukari kutoka kiwandani hapo.

Kiwanda hicho cha Sukari cha Kagera kiko katika sehemu Kaskazini Magharibi ya Tanzania (karibu na mpaka wa Tanzania na Uganda) kilibinafsishwa na Serikali kwa sekta binafsi mwaka 2001. Malengo ya ubinafsishaji yalikuwa kuboresha upanuzi wa masoko ya ndani na kikanda, uwekezaji wa kisasa, upanuzi na ukarabati na majengo ili kuhakikisha shughuli za kiundeshaji zinaboreshwa.

Daraja la Mto Kagera.

Mto wa Kagera ni kati ya mito inayounda mto wa Nile pia ni mto mkubwa kabisa wa kuingia ziwa la Viktoria Nyanza. Inaanza Burundi inapounganika mito ya Nyawarongo na Ruvuvu ikiendela 400 km hadi kuingia ziwa la Victoria Nyanza. 

Mto wa Kagera ukielekea kaskazini ni mpaka kati ya Tanzania na Rwanda; pale inapogeuka kuelekea mashariki karibu na mji wa Kikagati ni mpaka kati ya Tanzania na Uganda. Sehemu ya mwisho wa njia yake inaingia kabisa ndani ya eneo la Tanzania hadi kufika Viktoria Nyanza kama 40 km kaskazini za Bukoba. Jina la Mto wa Kagera umekuwa pia jina la mbuga ya wanyama ya Akagera National Park huko Rwanda na pia la Mkoa wa Kagera katika Tanzania.
Wanafunzi wa hao wa darasa la saba walipata nafasi wakapita Darajan hapo na kuweza kujionea taswira kamili ya Daraja hilo. Wengi wa Wanafunzi hao walikuwa hawajawahi kupita hapo. Habari na Picha na Faustine Ruta, Bukoba

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA