Vijana 2,100 wakiwemo 32 wa kutoka Musoma Vijijini, walianza matembezi ya miguu kutokea Butiama hadi Mwanza siku ya Jumatano, 9.10.2024.
Matembezi haya yanafuata nyayo za matembezi ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyoyafanya Mwaka 1967 akiunga mkono Azimio la Arusha lililozaliwa mwaka huo (1967)
Vilevile, matembezi haya ni sehemu ya sherehe za kilele cha ukimbizaji Mwenge wa Uhuru zitakazohitimishwa Jijini Mwanza tarehe 14.10.2024
CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa inaelezea baadhi ya matukio ya tarehe 9.10.2024 ya Kijijini Butiama - tafadhali isikilize.
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz
Comments