🟩🟨⬛️MZIZE HATOISAHAU SIKU YA LEO. Siku moja tu imebadili kila kitu na kumpa rekodi 3 za kutisha🔥🔥🔥 🔰...Achilia mbali rekodi ya kuivusha Tanzania kwenda robo fainali ya michuano ya #chan2024, achana na rekodi ya kubeba tuzo ya Man Of The Match leo,,, Hizi hapa rekodi 3 za kutisha za Clement Mzize mpaka sasa.... ✅TOP SCORER Mpaka sasa ukienda kwenye orodha ya wafungaji mabao kwenye michuano ya CHAN 2024, utalikuta jina la Mzize pale juu akiwa na mabao mawili sawa na Austin Odhiambo wa Kenya🇰🇪, ila huyu yeye ana bao moja la penati hivyo Mzize ni namba☝️ ✅MCHEZAJI WA KWANZA KUFUNGA MABAO MAWILI KWENYE MECHI MOJA. Yeees! Hakuna na hakuna tena mchezaji mwingine yeyote aliyebahatika kufunga mabao mawili kwenye mchezo mmoja wa michuano hii ya CHAN 2024. Ni Mzize pekee ✅MCHEZAJI PEKEE ALIYEFUNGA MABAO MAWILI NDANI YA MUDA MFUPI ZAIDI. Mzize leo amefunga mabao yake mawili ndani ya dakika 7 tu, akifunga bao la kwanza mnamo dakika ya 13 ya mchezo kisha akarudia kufanya hivyo dakika ya 20. Hivyo Mzize amehitaji dakika 7 tu leo kuionesha Afrika kwamba hacheki na wowote. ◇Hizo ni rekodi tatu kubwa za Mzize alizozipata leo tu. Hakika @clementinho49 hatoisahau siku ya leo, 09.08.2025. Vipi umemtazama leo ukiwa wapi? #chan2024 #nelloveupdates #daimambelenyumamwiko

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

WALIOKUWA WABUNGE WALIOPITIWA NA MKASI WA WAJUMBE

MWANAUME USIPITWE NA HILI, INASIKITISHA...?!!!

USAJILI ULIVYO HADI SASA....

SPIKA MSTAAFU NDUGAI AFARIKI DUNIA

RAIS SAMIA AYATAKA MASHINDANO YA MISS WORLD 2027

MAMBO 7 MUHIMU YA KUYAEPUKA BAADA YA KUACHANA...

MWENYE MASIKIO NA ASIKIE....

RAIS SAMIA AMUONDOLEA POLEPOLE HADHI YA UBALOZI