AZAM FC YAZIDI KUNG’ARA LIGI KUU, YAITANDIKA KAGERA SUGAR 2-0, TOTO YALALA 1-0 NYUMBANI


MATOKEO NA RATIBA LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA
Leo; Desemba 27, 2015
Azam FC 2-0 Kagera Sugar
Toto Africans 0-1 African Sports
Jana; Desemba 26, 2015
Ndanda FC 1 - 3 JKT Ruvu
Yanga SC 3 - 0 Mbeya City
Majimaji 0 - 2 Prisons
Mwadui FC 1 - 1 Simba SC
Mtibwa Sugar 3 - 0 Mgambo JKT
Coastal Union 1 - 3 Stand United
MECHI ZIJAZO;
Desemba 30, 2015
Azam FC vs Mtibwa Sugar
Januari 1, 2015
Ndanda FC vs Simba SC
Shomary Kapombe wa Azam FC (katikati) akikimbia baada ya kuifungia timu yae bao a pili, huku kipa wa Kagera Sugar, Agathon Anthony akiwa anashuhudia mpira ukitinga nyavuni 

Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
AZAM FC imeendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya jioni ya leo kuifunga Kagera Sugar mabao 2-0 Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Ushindi huo, unaifanya timu hiyo ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake ifikishe pointi 32 baada ya kucheza mechi 12, ikizidiwa pointi moja na mabingwa watetezi, Yanga SC wenye mchezo mmoja zaidi.
Mabao ya mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati leo yamefungwa na mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche na beki mzalendo, Shomary Salum Kapombe.
Tchetche alifunga bao la kwanza kwa kichwa dakika ya tisa, akimalizia kona maridadi iliyochongwa na kiungo Himid Mao Mkami ‘Ninja’.
Kipa Aishi Manula alicheza kwa mguu mkwaju wa penalti wa Nahodha wa Kagera Sugar, Salum Kanoni Kupela dakika ya 35, baada ya beki Msenegali, Racine Diouf kumuangusha Ramadhani Kiparamoto kwenye eneo la hatari.
Kapombe aliifungia Azam FC bao la pili dakika 74 baada ya kupasua katikati ya mabeki wa Kagera kufuatia kutanguliziwa pasi nzuri na Himid Mao.
Mchezo mwingine wa Ligi Kuu leo, Toto African imefungwa 1-0 nyumbani na African Sports ya Tanga Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.
Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni/Abdallah Kheri dk34, Serge Wawa, Kipre Bolou/Ramadhani Singano ‘Messi’, Racine Diouf, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Himid Mao, Kipre Tchetche, John Bocco/Farid Mussa dk46 na Didier Kavumbangu. 
Kagera Sugar: Antony Agaton, Salum Kanon, Juma Jabu, Erick Kyaruzi, Shaban Ibrahim, Mbaraka Yusuph, Daud Jumanne, Martim Lupart, Ramadham Kiparamoto na Pauj Ngwai/Adam Kingwande dk58.
 
Kwa hisani ya Bin Zubeiry Blog

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

CPA MAKALLA 'KUUTEKA' MKOA WA ARUSHA

𝗠𝗕𝗢𝗪𝗘 𝗔𝗦𝗜𝗧𝗜𝗦𝗛𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗗𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗬𝗔 𝗖𝗛𝗔𝗗𝗘𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗧𝗔𝗥𝗘𝗛𝗘 𝟮𝟯.

DEMU KAMA ANAFANYA KAZI HIZI KUWA MAKINI NAE.

ASKOFU CHANDE AISHUKURU SERIKALI KULIPATIA USAJILI WA KUDUMU KANISA LA KARMELI

JENGENI UWANJA WA MICHEZO WA KISASA NJOMBE-MWANYIKA