Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini, Deodatus Mwanyika (kushoto) akijadiliana jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Hamad Abdallah kwenye viunga vya Bunge Mei 28, 2026. ............. Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika hilo ikiambatana na Menejimenti ya Shirika hilo iliwahi tembelea mkoa wa Njombe kujionea fursa mbalimbali za uwekezaji katika sekta ya makazi na biashara. Ziara hiyo ilifanyika kwa ushirikiano na Kamishna wa Ardhi wa Mkoa wa Njombe pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Bw. Christopher Aloyce Sanga. Kupitia ziara hiyo, Bodi ilipata nafasi ya kuona maeneo ambayo Halmashauri ya Wilaya ya Njombe inapendekeza kushirikiana na NHC katika kuendeleza miradi ya kimkakati ya majengo ya biashara na nyumba bora za kisasa. Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Bw. Hamad Abdallah, alisema NHC inatambua Njombe kama mkoa wenye...
- Get link
- X
- Other Apps