NA MWANDISHI WETU RAIS Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania na Singapore zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika biashara, uwekezaji, maendeleo ya vijana, uchumi wa kidijitali na usalama wa chakula kufuatia mazungumzo ya kihistoria yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Makubaliano hayo yamefikiwa wakati wa ziara ya kwanza ya kiserikali ya Rais wa Singapore, , nchini Tanzania, hatua ambayo pia imeadhimisha miaka 45 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili. Akizungumza baada ya mazungumzo rasmi, Rais Samia alisema Tanzania na Singapore zimefanya tathmini ya ushirikiano uliopo na kukubaliana kuendelea kushirikiana zaidi ili kuleta manufaa makubwa kwa wananchi wa nchi zote mbili. Alisema kiwango cha sasa cha biashara kati ya Tanzania na Singapore kinakadiriwa kufikia dola za Marekani milioni 299 huku Singapore ikiwa na miradi 36 ya uwekezaji nchini Tanzania, kiwango ambacho hakilingani na ukubwa wa urafiki uliopo kati ya mataifa hayo. "Tumekubaliana kuongez...
- Get link
- X
- Other Apps