Na Victor Masangu,Pwani Jumuiya ya umoja wa wanawake (UWT) Mkoa wa Pwani imeamua kuwajengea uwezo na maharifa madiwani wote wa viti maalumu kwa kuwapatia semina elezeki ambayo itawasaidia katika kutekeleza majukumu yao. Katika semina hiyo ambayo pia imehudhuliwa na makatibu wa UWT ngazi za Wilaya imelenga kuwajengea uwezo ikiwa pamoja na kuwakumbusha wajibu na majukumu yao ya kila siku ya ndani ya chama na jumuiya. Katibu wa jumuiya ya wanawake (UWT) Mkoa wa Pwani Aziza Hussein amebainisha kwamba katika semina hiyo madiwani wamekumbushwa katika suala la kusimamia miradi ya maendeleo. Pia katibu huyo amesema kwamba madiwani hao wameweza kupatiwa mbinu mbali ambazo zitaweza kuwasaidia katika kutatua changamoto ambazo zinawakabili wananchi. "Tumeandaa semina hii ya kuwakutaniisha madiwani wote wa viti maalumu kutoka Mkoa wetu wa Pwani na lengo kubwa ni kuwajengea uwezo wa kutatua mambo mbali mbali ambayo wamekuwa wakiyatekeleza katika maeneo yao,"amebain...
- Get link
- X
- Other Apps