Wizara Viwanda na Biashara kupitia FCC imeendelea na juhudi za kupambana na bidhaa bandia na kumlinda mlaji dhidi ya mienendo potofu, hadaifu na kandamizi katika soko la bidhaa na huduma. Hayo yameelezwa na Waziri wa wizara hiyo, Judith Kapinga alipokuwa akiwasilisha hotuba ya makadirio ya Bajeti ya wizara kwa mwaka wa fedha wa 2026/2027 bungeni Dodoma Mei 22, 2026. Amesema hadi kufikia Aprili, 2026, Wizara kupitia FCC imeshughulikia malalamiko 63 ya walaji wadogo ambapo malalamiko 45 yalipatiwa ufumbuzi na malalamiko 18 yaliyobaki yapo katika hatua mbalimbali za utatuzi; Aidha, Waziri Kapinga amesema kuwa FCC imesajili na kuthibitisha mikataba 27 inayoandaliwa na upande mmoja (SFCC) kwa lengo la kuondoa masharti kandamizi kwa walaji; "FCC imefanya kaguzi za kushtukiza 31 ambapo bidhaa zenye thamani ya shilingi bilioni 4.74 zilikamatwa kwa kuvunja Sheria ya Alama za Bidhaa ya 1963 (kama ilivyorekebishwa). " Ametaja bidhaa zilizokamatwa kuwa ni; vipuri vya magari,...
- Get link
- X
- Other Apps