WAZIRI Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda, ameongoza shughuli ya upandaji wa takribani miti 7,000 katika eneo la Ndejengwa jijini Dodoma, ikiwa ni hatua ya kuelekea utekelezaji wa mradi wa kuanzisha Msitu wa Mjini (Urban Forest) utakaohusisha upandaji wa miti 20,000 katika Jiji la Dodoma. Shughuli hiyo imeandaliwa na Habari Conservation Organisation (HCO) kwa ufadhili wa East African Crude Oil Pipeline (EACOP) na ni sehemu ya kampeni ya "Kijanisha Dodoma" iliyoasisiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipokuwa Makamu wa Rais. Akizungumza baada ya kushiriki upandaji wa miti hiyo, Pinda amesema uanzishwaji wa misitu ya mijini ni hatua muhimu katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, kupunguza ongezeko la joto, kuhifadhi vyanzo vya maji na kuboresha mazingira ya makazi. Amesema ukuaji wa miji unapaswa kwenda sambamba na uwekezaji katika maeneo ya kijani ili kuhakikisha maendeleo yanakuwa endelevu. "Hatupaswi kupanda miti tu, ...
- Get link
- X
- Other Apps