JUMUIYA ya Umoja wa Wanawake ya Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT), imetoa msaada wa vifaa tiba katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma ikiwa ni moja ya shamrashamra ya kuadhimisha miaka 49 ya kuzaliwa kwa chama hicho. Akitoa msaada huo kwa niaba ya Mwenyekiti wa UWT, Mary Chatanda, Katibu Mkuu wa UWT, Suzani Kunambi amesema kuwa vifaa hivyo vyenye thamani ya sh. mil. 20 ni maalumu kwa ajili ya Wodi za wajawazito na watoto Njiti. Ametaja vifaa hivyo vilivyopokelewa na Mganga Mfawidhi msaidizi wa hospitali hiyo, Sara Ludovick kuwa ni; vitanda, mashine za kuleta joto kwa watoto Njiti, sabuni, mafuta na khanga. Katibu Mkuu na wajumbe alioambatana nao walipata wasaa wa kuwatembelea wodi za wazazi na watoto njiti na kuwagapatia wazazi baadhi ya vifaa hivyo pamoja na vitu hivyo vingine. Kunambi ambaye aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, baadhi ya viongozi wa UWT Taifa, UWT Mkoa wa Dodoma, Wilaya ya Dodoma walipanda miti kwenye viunga vya hospitali hiyo. ...
- Get link
- X
- Other Apps