Na Richard Mwaikenda, Dodoma Waziri Mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda ameongoza kupanda miti 1000 katika eneo la Ndejengwa jijini Dodoma leo Februari 6, 2026. Katika shughuli hiyo iliyoandaliwa na Taasisi ya Habari Conservation,Mzee Pinda ambaye ni mlezi wa taasisi hiyo aliongozana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ambaye pia alipanda mti wa kumbukumbu. Pia walishiriki wanafunzi na wananchi wanaoishi karibu na eneo hilo wazi ambalo kwa mujibu wa Afisa Habari wa Taasisi hiyo, Loyce Joseph amesema wataligeuza kuwa msitu wenye miti ya kivuli na matunda jambo ambalo litakuwa linavutia watu kwenda kutembelea na kufanya sherehe zao ndogo ndogo. Shughuli hiyo imedhaminiwa kwa asilimia kubwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) ambayo Mkurugenzi wake Mkuu ni CPA. Dennis Simba ambaye pia yeye na watumishi wake walishiriki kupanda miti. Mzee Pinda, na Mkuu wa Mkoa Senyamule wameipongeza taasisi hiyo inayoongozwa kwa asilimia kubwa ...
- Get link
- X
- Other Apps