NA: MWANDISHI WETU, DODOMA Wito umetolewa kwa wanawake nchini kuwa sehemu ya hamasa ya kuelimisha jamii kuepuka uchochezi wa kufanya maandamano badala yake waitunze tunu ya amani iliyopo. Hayo yameelezwa na Mwenyekiti Taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Chatanda, Julai 3, 2026, Jijini Dodoma. Amesema, kama ambavyo ukimwelimisha mwanamke umeelimisha jamii nzima, hivyo mwanamke akisimama imara atakuwa sehemu ya kuepusha maandamano yanayoratibiwa na baadhi ya wanasiasa na wanaharakati, Julai 7. "Leo, nina ujumbe mahsusi kwa wanawake wenzangu. Nina wajibu wa kuongea na wanawake na wananchi kwa ujumla juu ya kutunza tunu ya amani tuliyonayo. Wanawake, hebu tukae chini na waume zetu, tuwaelimishe umuhimu wa amani na kuepuka maandamano". "Kimsingi, shughuli wanazofanya za kuingiza vipato ambavyo tunapata chakula na mahitaji muhimu ya watoto wetu wanaosoma shuleni na vyuoni hazitafanyika katikati ya vurugu na maandamano," amesema Chatanda. Aidha, Chatanda amesem...
- Get link
- X
- Other Apps