1. Usimfanye kuwa dunia yako yote Mapenzi ni mazuri, lakini usifikie hatua ya kusahau marafiki, familia, kazi au malengo yako kwa sababu ya mwanaume. Ukimzungusha maisha yako yote kwake, unaweza kuumia sana endapo mambo yatabadilika ghafla. 2. Usitoe kila kitu huku yeye hatoi chochote Kama wewe ndiye unajitolea muda, pesa, nguvu na upendo kila siku huku yeye akipokea tu, simama na kutafakari. Mahusiano yanahitaji usawa wa kujitolea kutoka pande zote mbili. 3. Usikubali dharau kwa jina la mapenzi Mwanaume anayekudhalilisha mbele za watu, anayekutukana au kukufanya ujisikie huna thamani hafanyi hivyo kwa sababu anakupenda. Heshima ni msingi wa mapenzi ya kweli. 4. Usiachane na ndoto zako kwa ajili yake Kuna wanawake huacha masomo, biashara au kazi wakiamini mwanaume atawajengea maisha bora. Endelea kujijenga. Mwanaume mzuri atakuunga mkono kufikia ndoto zako, si kuzizima. 5. Usimpe mamlaka ya kuamua furaha yako Furaha yako isitegemee meseji zake, simu zake au uwepo wake pekee. Jifunze ku...
- Get link
- X
- Other Apps