Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, inayoadhimishwa kila mwaka Machi 8, wanawake wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) wametoa msaada wa mifuko 50 ya saruji, matofali 1,000 pamoja na mahitaji mbalimbali ya watoto katika Kituo cha kulea watoto yatima na waliofanyiwa ukatili cha Shalom kilichopo Kidenge B, Kata ya Msangani, Halmashauri ya Mji wa Kibaha, mkoani Pwani Machi 6, 2026. Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Meneja wa Udhibiti na Viwango wa Mamlaka hiyo Bi. Sultana Seiff, alisema kuwa wanawake wa e-GA wameamua kusherehekea siku hiyo kwa kuwafikia watoto wanaohitaji msaada katika jamii na kukichagua kituo hicho ikiwa kama sehemu ya kurudisha kwa jamii. Meneja huyo alisema kuwa baada ya kuwasiliana na kituo hicho na kupata changamoto mbalimbali zinazohitaji kutatuliwa katika kituo hicho ikiwemo ujenzi wa uzio ili kuhakikisha Watoto hao wanakua salama waliamua kuchangia vifaa vya ujenzi pamoja na mahitaji mengine muhimu kwa Watoto...
- Get link
- X
- Other Apps