NA MWANDISHI WETU, ARUSHA MRADI wa Kilimo Endelevu unaotekelezwa kwenye vijiji vya Seuri na Oldonyowas mkoani hapa, umeepusha wakulima na mikopo ‘kausha damu’. Mradi huo unafadhiliwa na Shirika la Island of Peace (IDP) na lingine lisilo la Serikali linalojihusisha na utafiti, ushauri wa kitaalamu na Miradi ya Maendeleo na Jamii (RECODA) ukinufaisha zaidi ya wakulima 700 wa vijiji 10. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti, wakulima wa vijiji hivyo walisema walishakata tamaa na kilimo, kutokana na mavuno madogo waliyokuwa wakipata, ila tangu mradi huo uanze, wanaona matumaini mapya. Mkulima Witness Sikoi wa Seuri, amesema IDP na RECODA wamemfanya aone kilimo kinalipa, kutokana na hatua aliyopiga. Witness, Mwenyekiti wa Kikundi cha Elishorie, amesema kabla ya mradi wa Kilimo Endelevu wanawake wengi walishiriki mikopo inayotesa na kuwagombanisha na waume zao. "Hatukuwa na amani kutokana na mikopo ya kausha damu, ila kwa sasa tuna amani isiyo na kifani, kwani tun...
- Get link
- X
- Other Apps