Afrika na Waafrika ni lazima tuamke. Tumelala mno! Tuliuzwa sokoni kama bidhaa wakati wa utumwa; Tulinyonywa, kukandamizwa na kuvuliwa utu wetu, wakati wa ukoloni; Tumeendelea kuhadaiwa na mfumo wa ukoloni mamboleo, kwamba sisi ni maskini tunaohitaji kusaidiwa; Unasaidiwaje na walewale waliokuuza sokoni kama kuku, wakati walikuja kuiba rasilmali zako, ambazo wanazihitaji na kuzifuata hadi leo? Tafiti zinathibitisha kuwa kila Shilingi moja inayokuja Afrika kama msaada, wao wanachukua Shilingi mbili!Hapa ni nani anamsaidia mwingine? Imekuwaje leo, wasomi wa Afrika hawazungumzii kwa sauti suala hili, wakati liko wazi? Je, ni kwa sababu wanalamba asali ya mabeberu? Inakuwaje John Perkins, ktk vitabu vyake vya 'Confessions of an Economic Hitman' anaeleza wazi michezo wanayoicheza mabeberu Afrika na bado Waafrika hawaelewi na hawaamki? Je, ni kwamba Waafrika ni watu wasioweza kung'amua mambo au ni kwamba wamepigwa juju na mabeberu? Je, ni kwa nini ktk historia niliyosoma kuhusu...
- Get link
- X
- Other Apps