NA OWM TAMISEMI, MOROGORO Tanzania imeandika historia katika Mashindano ya FEASSA Games 2026 baada ya kushiriki kwa mara ya kwanza katika mbio za kuruka vihunzi na kufanikiwa kutwaa nafasi ya tatu. Mashindano hayo yaliyofanyika katika Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, yameshuhudia wanariadha wa Tanzania wakionesha ushindani mkubwa na kupeperusha vyema bendera ya Taifa. Katika mbio hizo, Magrita IQamunga alimaliza katika nafasi ya tatu, huku Winfrida Urbano akishika nafasi ya nne, matokeo yanayoonesha uwezo na vipaji vinavyoendelea kukua katika riadha nchini. Mafanikio hayo yameongeza hamasa kwa Tanzania katika FEASSA Games 2026, huku ushiriki wa kwanza katika mbio za vihunzi ukiwa hatua muhimu katika kukuza na kuibua vipaji vipya vya riadha miongoni mwa wanafunzi. Tanzania inaendelea kuonesha ushindani katika michezo mbalimbali ya FEASSA 2026, huku vijana wakipeperusha bendera ya Taifa kwa bidii, nidhamu na ari ya ushindi.
- Get link
- X
- Other Apps