NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imewataka Wamiliki wa Mabasi kuhakikisha madereva, Utingo na wahudumu wao wanafuata sheria ambazo zimewekwa na Serikali za kupokea na kusafirisha mizigo. Imeelezwa sheria hizo zitasaidia kuzuia matumizi ya vyombo hivyo kusafirisha dawa za kulevya na kusisitizwa kwamba kila kifurushi kinapaswa kutambulika mmiliki wake na kuwepo taarifa sahihi za mtumaji na mpokeaji. Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo, amebainisha hayo, leo Juni 12, 2026 katika Kituo Kikuu Cha Mabasi Magufuli (Magufuli Terminal), Mbezi jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa filamu iliyotayarishwa kwa lengo la kutoa elimu kwa umma kuhusu athari za biashara na matumizi ya dawa za kulevya. "Hatua hiyo itasaidia kubaini wahusika endapo mzigo haramu utagundulika na kuondoa uwezekano wa kuwahusisha watu wasiohusika na uhalifu huo. Ameongeza kwamba kubeba vifurushi visivyojulikana kunaweza kusababisha madhara ya kisheri...
- Get link
- X
- Other Apps