Na Mwandishi Wetu - Mbeya 16/8/2027 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI)Dkt. Diwani Msemo amesema kukamilika kwa ujenzi wa Kituo cha Saratani ORCI Mbeya kutakuwa ni hatua muhimu katika kutimiza azma ya Serikali ya kusogeza huduma za kibingwa na kibobezi za saratani karibu na wananchi wa Nyanda za Juu Kusini na nchi jirani. Dkt. Msemo amesema Serikali imewekeza takribani Shilingi bilioni 11 katika ujenzi wa kituo hicho ambacho kinatarajiwa kukamilika Januari 2027 na kuongeza uwezo wa kutoa huduma za uchunguzi, tiba na ufuatiliaji wa wagonjwa wa saratani katika ukanda huo. Akizungumza wakati wa ziara ya wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya ORCI katika mradi huo jijini Mbeya, Dkt. Msemo amesema ujenzi wa vituo vya kikanda ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kupanua huduma za saratani nchini huku ORCI ikiwa na jukumu la kusaidia kusambaza huduma za kibingwa na kibobezi katika maeneo mbalimbali. Amesema hatua hiyo inalenga kupunguza...
- Get link
- X
- Other Apps