Na Victor Masangu, Pwani Serikali ya awamu ya sita katika kupambana na changamoto ya ukosefu wa ajira imeamua kuja na mpango kabambe wa kuanzisha shindano linalojulikana kwa jina la Vijana uchumi Challenge lenye lengo la kuwakutanisha vijana mbali mbali ili waweze kutoa kutoa mawazo yenye kuleta tija katika kuisaidia serikali katika nyanja mbali mbali ikiwemo uchumi na maendeleo. Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Ofisi ya Rais maendeleo ya vijana Dkt. Kedmon Mapana wakati wa halfa ya uzinduzi rasmi wa kambi maalumu kwa ajili ya usahili wa vijana wapatao 100 bora ambao wamepata fursa ya kuchaguliwa kati ya vijana elfu 7852 walioshiriki hapo awali kutoka mikoa mbali mbali ipatayo 27 ya Tanzania bara na visiwani. Pia amebainisha kwamba ana imani vijana hao 100 ambao wamechaguliwa na kuweka kambi wataweza kuleta matokeo chanya na kwamba serikali itaendelea kushirikiana nao bega kwa bega na kuchukua mawazo yao ambayo watakwenda ku...
- Get link
- X
- Other Apps