Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa (MCC), Mary Chatanda amesema mageuzi makubwa ya kimaendeleo yaliyofanywa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan yamekuwa chachu ya vyuo vikuu vya ndani na nje ya Tanzania kumtunuku Shahada mbalimbali za Heshima za Uzamivu. Chatanda ametoa kauli hiyo Juni 5, 2026, Jijini Dodoma ikiwa ni siku moja imepita tangu Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi (RADN University) kumtunuku Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa), Jijini Moscow, Urusi. "Unajua utendajikazi mzuri wa Rais wetu Dk. Samia unaonekana duniani kote, na wengi wanaridhishwa na juhudi kubwa zinazofanywa ana serikali katika kuchochea maendeleo ya nchi. Rais amefanya mageuzi makubwa ya kimaendeleo, na ndiyo maana wenzetu wa Urusi wamemtunuku Shahada ya Udaktari wa Heshima," amesema Chatanda. Sambamba na hilo, Chatanda amesema katika kila sekta, kuna mabadiliko chanya mengi ambayo yamefanyika ndani ya muda mfupi, ndiyo maana hata mataifa...
- Get link
- X
- Other Apps