NA OWM-TAMISEMI,MOROGORO Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema michezo ni nyenzo muhimu ya kujenga amani, umoja na mshikamano, kwa kuwa huwaunganisha watu bila kujali tofauti za kisiasa, kiutamaduni au mipaka ya nchi. Prof. Mkenda ameyasema hayo leo, Agosti 16, 2026, wakati wa ufunguzi wa Mashindano ya Michezo ya Wanafunzi wa Shule za Afrika Mashariki (FEASSA Games 2026) kwa niaba ya Waziri Mkuu Dkt.Mwigulu Nchemba yanayofanyika mkoani Morogoro. Amesema FEASSA si mashindano ya kutafuta medali pekee, bali ni jukwaa la kukuza vipaji, kujenga urafiki na kuimarisha umoja wa vijana wa Afrika Mashariki. Amesisitiza kuwa kupitia michezo, wanafunzi hujifunza nidhamu, heshima, ushirikiano na uvumilivu, mambo ambayo ni msingi wa kujenga kizazi chenye uwezo wa kuleta maendeleo katika nchi zao na Afrika Mashariki kwa ujumla. “Michezo inatufanya tushindane uwanjani, lakini tubaki kuwa marafiki nje ya uwanja,” amesema Prof. Mkenda. Ameeleza kuwa Serikali itaendelea...
- Get link
- X
- Other Apps