Benki ya NMB imeendelea kuifanya Nanenane 2026 kuwa zaidi ya maonesho ya kilimo kwa kuendesha kampeni ya utoaji wa elimu ya kifedha, ujasiriamali na usimamizi wa biashara kwa wananchi waliotembelea mabanda yake katika kanda mbalimbali nchini. Katika Banda la Vijana lililopo viwanja vya DK John Mwakangale jijini Dodoma, vijana wa mradi wa Building a Better Tomorrow (BBT) walipata mafunzo kuhusu namna ya kugeuza mawazo yao kuwa biashara endelevu, kusimamia fedha na kutumia huduma za kifedha kukuza shughuli za kilimo, ufugaji na uvuvi. Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mkuu wa Idara ya Kilimo kwa Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Christopher Mwalungenge, aliwahimiza vijana kuona kilimo kama biashara yenye fursa kubwa za kujenga kipato, ajira na ustawi wa muda mrefu. Mbali na vijana, maafisa wa NMB waliendelea kutoa elimu kwa vikundi vya wakulima, wafugaji na wajasiriamali waliotembelea mabanda ya benki hiyo. Washiriki walipata uelewa kuhusu huduma za kifedha, mi...
- Get link
- X
- Other Apps