NA MWANDISHI WETU, MOROGORO MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza ekari 603 za mashamba ya bangi na kukamata magunia 49 ya bangi katika operesheni maalum iliyofanyika Wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro, huku watuhumiwa 13 wakikamatwa kuhusisiana na mashamba hayo. Operesheni hiyo iliyofanyika katika vijiji vya Misengele, Lugenge, Kisaki na Nyarutanga, pia ilibaini na kuharibu kambi 21 zilizokuwa zikitumiwa na wakulima wa bangi. Akizungumza jana kuhusu operesheni hiyo, Kamishna Jenerali wa DCEA Aretas Lyimo, amesema hatua hiyo ni sehemu ya mkakati endelevu wa Serikali wa kudhibiti uzalishaji wa dawa za kulevya nchini, hususan bangi, ambayo imeendelea kuzalishwa katika baadhi ya maeneo ya nchi. Amesema operesheni hizo zimebaini mabadiliko katika mbinu zinazotumiwa na baadhi ya wakulima wa bangi, ambapo wanahamisha shughuli zao kutoka maeneo yaliyofikiwa na operesheni na kuingia ndani zaidi ya maeneo ya hifadhi. “Tumebaini kuwa baadhi ya wakulim...
- Get link
- X
- Other Apps