Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amewataka wanawake wa Jeshi la Magereza kuendelea kujijengea uwezo, kuongeza elimu na ujuzi ili kupata nafasi mbalimbali za uongozi na kitaaluma katika Jeshi hilo, huku akisisitiza umuhimu wa kuendana na mabadiliko ya teknolojia na fursa za kidijitali katika utekelezaji wa majukumu yao. Mhe. Mahundi ametoa kauli hiyo, Septemba 07, 2026 jijini Dodoma, wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Mtandao wa Wanawake Jeshi la Magereza Tanzania 2026, unaolenga kuwajengea uwezo wanawake, kukuza uongozi, kuimarisha usawa wa kijinsia na kuongeza ufanisi katika majukumu ya urekebishaji wa wafungwa. Amesema uwezeshaji wa wanawake ni sehemu muhimu ya kujenga mtaji watu wenye uwezo, akiwataka wanawake wa Jeshi la Magereza kuwa mstari wa mbele katika mageuzi ya kijamii na kidijitali ya Jeshi hilo. “Nawahimiza wanawake wa Jeshi la Magereza kujiamini, kuongeza elimu na ujuzi, na kujiandaa kwa ushin...
- Get link
- X
- Other Apps