WIZARA YA ELIMU NA COSTECH KWA KUSHIRIKIANA NA BENKI YA CRDB WATENGA SHILINGI BILIONI 4.6 KUWAWEZESHA VIJANA WABUNIFU
WIZARA YA ELIMU NA COSTECH KWA KUSHIRIKIANA NA BENKI YA CRDB WATENGA SHILINGI BILIONI 4.6 KUWAWEZESHA VIJANA WABUNIFU
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na Benki ya CRDB imetenga jumla ya Shilingi bilioni 4.6 kwa ajili ya kuwawezesha mitaji vijana wabunifu waliofikia hatua ya kupeleka bidhaa na huduma zao sokoni. Uwezeshaji huo unafanyika kupitia Mfuko wa Samia wa Ubiasharishaji Ubunifu uliozinduliwa mwaka 2024, ambao umetambua jumla ya wabunifu 3,300 nchini, ambapo kati yao 300 wameendelezwa kupitia Mfuko wa Taifa wa Uendelezaji Sayansi na Teknolojia (MTUSATE) unaosimamiwa na COSTECH. Akizungumza Februari 13, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kuwatambua wanufaika saba waliopata mikopo ya masharti nafuu kupitia mfuko huo, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidhi Ameir, amesema Serikali imeielekeza Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kuhakikisha wabunifu, ambao wengi wao ni vijana, wanawezeshwa kukabiliana na ushindani wa soko. Amesema uwekezaji huo unawalenga watanzania wenye bunifu zil...
- Get link
- X
- Other Apps