Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus C. Sangu, akizungumza na waandishi wa habari mjini Sumbawanga, Mkoa wa Rukwa, leo Julai 23, 2026,kuhusu Tanzania kushiriki katika maonesho ya Wajasiliamali Wadogo (Juakali) ya Afrika Mashariki yatakayofanyika Kigali Rwanda mwezi Oktoba mwaka huu. Na: Mwandishi Wetu, SUMBAWANGA Serikali imetangaza kuwa Tanzania itashiriki Maonesho ya 26 ya Wajasiriamali Wadogowadogo, Wadogo na wa Kati (MSMEs) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, maarufu kama Nguvu Kazi/Jua Kali, yatakayofanyika jijini Kigali, Rwanda kuanzia Oktoba 30 hadi Novemba 8, 2026. Akitoa taarifa kwa umma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, amesema Tanzania itawakilishwa na wajasiriamali 250 kati ya washiriki wapatao 1,000 wanaotarajiwa kutoka nchi nane wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Amesema kaulimbiu ya maonesho ya mwaka huu ni “Kuendeleza Mnyororo wa Thamani kwenye Sekta ya Ngozi na Kilimo cha B...
- Get link
- X
- Other Apps