NA MWANDISHI WETU, SIMIYU VIKUNDI vya Kijamii vinavyotekeleza matengenezo ya kawaida ya barabara kupitia Mpango wa CBRM unaotekelezwa na Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) vimetakiwa kushirikiana na wananchi katika kulinda na kutunza miundombinu ya barabara ili iweze kudumu na kuendelea kutoa huduma kwa jamii. Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Anna Gidarya wakati wa mafunzo yaliyowakutanisha jumla ya vikundi 16 kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kutekeleza kwa ufanisi shughuli za matengenezo madogo madogo ya barabara katika maeneo yao. Gidarya amesema barabara ni mali ya wananchi na ni sehemu muhimu ya kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii hivyo amewataka wanavikundi pamoja na wananchi kwa ujumla kuwa mstari wa mbele kuzilinda dhidi ya vitendo vinavyoweza kusababisha uharibifu wa miundombinu hiyo. Aidha, amevipongeza vikundi hivyo kwa kupata fursa ya kushiriki moja kwa moja katika matengenezo ya barabara akieleza kuwa hatua hiyo si t...
- Get link
- X
- Other Apps