Benki ya NMB imeendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za kuimarisha afya ya mwili na akili ya watumishi kupitia Mashindano ya Kitaifa ya SHIMISEMITA yanayoendelea mkoani Mbeya. Mashindano hayo yanawakutanisha zaidi ya watumishi 5,000 kutoka halmashauri 184 nchini, huku NMB ikiendelea kuwa miongoni mwa wadau wanaoyaunga mkono. Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu, Wogofya Mfalamagoha, alisema ushiriki wa benki hiyo unatokana na imani kwamba mtumishi mwenye afya ana nafasi kubwa ya kuwa na tija na kutoa huduma bora kwa wananchi. Katika mashindano ya mwaka huu, NMB imetoa Sh milioni 34.5 pamoja na jezi kwa timu zitakazofuzu hatua ya robo fainali katika mpira wa miguu, wavu, pete na kikapu. Mgeni rasmi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, aliyemwakilisha Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, aliipongeza NMB kwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika shughuli zinazochangia ustawi wa watumishi na wananchi. Alisema michezo inasaidia kujenga umoja na...
- Get link
- X
- Other Apps