Posts

NMB YAJIUNGA NA GOAT RACES KUCHAGiZA ELIMU YA VIJANA

  NMB Bank imejiunga kwa mara ya kwanza kuwa mdhamini wa Mbio za Mbuzi za mwaka 2026, zinazolenga kukusanya Sh milioni 200 kwa ajili ya kusaidia vijana 150 kujiunga na vyuo vikuu na mafunzo ya ufundi. Tukio hilo litafanyika Septemba 19 katika Viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Idara ya Wateja Maalum wa NMB Bank, Getrude Mallya, amesema uamuzi huo umetokana na uzoefu wa benki hiyo kama mshiriki wa tukio la mwaka jana pamoja na ulinganifu uliopo kati ya malengo ya Rotary na uwekezaji wa NMB katika elimu. NMB hutenga asilimia moja ya faida baada ya kodi kila mwaka kwa uwekezaji wa kijamii. Mwaka 2025, benki hiyo ilitoa madawati 6,365 kwa shule 124 nchini, hatua iliyonufaisha takribani wanafunzi 19,095. Rais wa Rotary Club of Dar es Salaam Oysterbay, Paul Muhato, amesema Sh milioni 163 kati ya Sh milioni 167 zilizokusanywa mwaka jana zimesaidia wanafunzi 136, wakiwemo 100 waliojiunga na vyuo vikuu na 36 waliojiunga na mafunzo ya ufundi.

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA NA MAWAZIRI WATOA POLE KWA RAIS SAMIA

HABARI ZILIZORINDIMA KATIKA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI SEPTEMBA 10, 2026

MFAHAMU LIA MUUAJI WA TANZANIA MWENYE ASILI YA KITANZANIA 🇹🇿

CLARA LUVANDA AVUNJA REKODI, ASAJILIWA KWA BIL. 5.28 MAREKANI

YANGA KUJENGA JENGO JWA SH. BIL. 5.5 KARIAKOO

NMB YAPANUA MALIPO YA KIDIJITALI KARIAKOO FESTIVAL

SALOME- NDEJEMBI, TUNAOMBA UENDELEE KUWA MLEZI WA WIZARA YA NISHATI

KIKWETE AHIMIZA TANZANIA NA JAPAN KUIMARISHA USHIRIKIANO KATIKA USALAMA WA CHAKULA NA UCHUMI WA BULUU

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

MATUKIO MBALIMBALI WAKATI WA KUAPISHWA NDEJEMBI KUWA MAKAMU WA RAIS

MAFAO YA MAKAMU WA RAIS ALIYEJIUZULU

NI MAKOSA WANAFUNZI KUFIKA SHULE SAA 1:15 ASUBUHI

URUSI, CHINA, IRANI NA KOREA KASKAZINI WAPANGA KUUNDA JESHI MOJA LA KUJIHAMI

𝐌𝐉𝐔𝐄 𝐊𝐀𝐂𝐇𝐄𝐑𝐎 𝐌𝐙𝐄𝐍𝐀

PANYA MAGAWA WA SUA TANZANIA AJENGEWA MNARA WA HESHIMA CAMBODIA