Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa, Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC), leo tarehe 14 Agosti 2026, amewaongoza viongozi na wanachama wa UWT kushiriki katika Kilele cha Tamasha la Kizimkazi, kilichofanyika katika Uwanja wa Mwembe Makunduchi, Zanzibar. Katika kilele hicho, Mwenyekiti Chatanda amewaongoza wana UWT katika shamrashamra za kusherehekea pamoja na wananchi na washiriki wengine wa tamasha hilo. Tamasha hilo limefungwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
- Get link
- X
- Other Apps