NA: MWANDISHI WETU, DODOMA Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu (MCC), Mary Chatanda, amempongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa kuunda Tume ya Kuchunguza Wahusika wa Ghasia za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025. Chatanda ametoa pongezi hizo, Agosti 09, 2026, Jijini Dodoma. Amesema, Rais Dk. Samia ameonyesha dhamira ya kujenga upya taifa lenye umoja na mshikamano, ndiyo maana ameunda Tume hiyo. "Kipekee nimpongeze Rais wetu, Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa kuunda Tume yenye wataalamu na wabobezi wa masuala mbalimbali ya kisheria wa ndani na nje ya nchi, naamini kwa Hadidu za Rejea walizonazo, watakuja na majibu ya maswali mengi waliyonayo wananchi," amesema Chatanda. Vilevile, amesema, ni vyema wananchi wakaiacha Tume hiyo ifanye kazi yake kwa mujibu wa sheria badala ya kuikosoa kabla ya kutekeleza kazi yake. "Ipo kasumba mbaya kwa baadhi ya watu kukosoa Tume inapoundwa hata kabla haijaanza utekelezaji w...
- Get link
- X
- Other Apps