Posts

KATIBU MKUU CCM, UJUMBE MTANDAO WA VIONGOZI WANAWAKE AFRIKA WAFANYA MAZUNGUMZO

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Asha-Rose Migiro, leo tarehe 21 Aprili 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Mtandao wa Viongozi Wanawake wa Afrika (African Women Leaders Network - AWLN), ulioongozwa na Marais wastaafu wa Jamhuri ya Liberia, Mhe. Ellen Johnson Sirleaf, na Jamhuri ya Shirikisho la Kidemokrasia ya Ethiopia, Mhe. Sahle-Work Zewde, jijini Dar es Salaam. Mazungumzo hayo yalijikita katika hali ya kisiasa nchini pamoja na matukio ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, yakihusisha pia umuhimu wa kudumisha amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa. Ujumbe huo upo nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kufanya mashauriano na viongozi mbalimbali wa kitaifa kuhusu maendeleo ya kisiasa na juhudi zinazoendelea za kuimarisha demokrasia na utawala bora, ikiwa ni sehemu ya mchango wa wanawake viongozi wa Afrika katika kulinda amani na utulivu barani.  

MAMBO YA BUNGENI DODOMA LEO

NMB YATOA SH. MIL. 100 KUDHAMINI MKUTANO MKUU WA 40 WA ALAT

FEDHA ZIMESAINIWA, UJENZI MRADI WA MAJI UTAANDA LINI - KASAKA

SERIKALI YAIMARISHA UPATIKANAJI WA MAFUTA YA PETROLI NCHINI MALAWI

SERIKALI KUTENGA ENEO LA VIWANDA VYA KUONGEZA THAMANI YA MAZAO YA MISITU, PARACHICHI

KUMBUKIZI YA DARAJA LA NYERERE 2016-2026

MATUKIO YA MBUNGE MWALUNENGE BUNGENI DODOMA

MWENGE WA UHURU KITAIFA KUPITIA JUMLA YA MIRADI 68 YENYE THAMANI YA BL.263.1 MKOA WA PWANI

DKT. RWEIKIZA APAMBANIA AJIRA ZA VIJANA

NMB YATOA SH. MIL 500 KUSAIDIA HUDUMA ZA UPANDIKISHAJI FIGO NA UBOHO BMH

MNEC-SUKI RABIA HAMIDI,KANSELA WA CPC WAFANYA KIKAO KAZI JIJINI DAR

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

Wasifu wa Kizza Besigye

AINA 10 ZA WANAWAKE AMBAO BIBLIA INAKUONYA UWAEPUKE

MAJANI YA MAPERA NA MATUMIZI YAKE YA KITIBA

UBORA UNAONEKANA: BENKI YA NMB YANG'ARA TUZO ZA EUROMONEY 2026

RAIS ALİYEISHI KAMA MUNGU WAKATI WATU WAKE WAKIFA NJAA

ZIJUE TIBA ZA MMEA WA MSHONA NGUO.