Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar akielezea mbele ya vyombo vya habari kuhusu maboresho ya kodi, ada na tozo mbalimbali, ambapo hadi wanafunga dirisha la kupokea maoni kwa mwaka 2026, jumla ya mapendekezo 727, ya kikodi, kisheria, na hata ya kiutawala yalipokelewa. Pamoja na mambo mengine, ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandhishi wa habari jijini Dodoma Juni 10, 2026, kuelezea kwa ufupi kuhusu mapendendekezo ya muelekeo wa Bajeti Kuu ya Serikali itakayowasilishwa rasmi bungeni kesho Alhamisi juni 11, 2026.. Amesema kuwa uchakataji wa mapendekezo hayo ulianza mwezi Februari 2026 kupitia Kamati ya Wataalam ya Maboresho ya Kodi (Taskforce on Tax Reforms) inayojumuisha wawakilishi kutoka Serikali Kuu, Taasisi zake na Sekta Binafsi. "Kati ya mapendekezo hayo, jumla ya mapendekezo 125 yalikubaliwa kama yalivyowasilishwa; 121 yalikubaliwa baada ya kuboreshwa; 295 yalikataliwa; mapendekezo 107 ilielekezwa na kamati ya maboresho ya mfumo wa kodi (Task Force on Ta...
- Get link
- X
- Other Apps