Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu wa Benki ya NMB, Erica Hanson (wapili kulia) akimkabidhi cheti cha uhitimu mwanafunzi, Irene Kimaro (wapili kushoto) wakati wa mahafali maalum ya mafunzo maalum ya utayari wa kuwa watumishi wa Benki (Graduate Bankers Readiness program) kutoka Benki ya NMB. Na Mwandishi Wetu Benki ya NMB imeendeleza jitihada zake za kujenga nguvu kazi yenye ujuzi na maarifa ya kisasa katika sekta ya fedha nchini kwa kusaidia mafunzo ya kitaaluma na kutalaamu kwa vijana 100 kupitia mpango maalumu wa mafunzo ya Graduate Banker Readiness Programme (GBRP) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kupitia mpango huo, Benki ya NMB kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, inatoa mafunzo, maarifa ya vitendo, na ufaham wa kina wa sekta ya fedha. Kundi la nne la mpango huu, kama ilivyokuwa kwa makundi yaliyotangulia, limepata mafunzo ya ujuzi muhimu, maarifa ya vitendo, na ufahamu wa kina wa sekta ya fedha, na lilihitimu Ijumaa iliyopita. Akizungumza kabla ya kuwa...
- Get link
- X
- Other Apps