DKT. BITEKO AKUTANA NA UJUMBE WA CHAMA CHA KIKOMUNISTI CHA VIETNAM*


 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko leo Septemba 23, 2024 amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kikao na Ujumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha Vietnam ukiongozwa na Mhe. Phan Dinh Trac kilichofanyika ofisini kwake jijini Dar es Salaam.


Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Biteko ameeleza kuwa Tanzania na Vietnam zimekuwa na uhusiano wa muda mrefu na zinaendelea kuimarisha uhusiano huo katika nyanja za diplomasia, siasa na uchumi. 


Aidha, ameipongeza Vietnam kwa kufanya uwekezaji nchini Tanzania ikiwemo katika Kampuni ya Simu za Halotel na kusema kuwa nchi hizo zinahitaji kuongeza kiwango cha biashara kati yake ambapo kiwango cha uwekezaji kwa sasa ni dola za kimarekani milioni 300.


Kwa upande wake, Mhe. Trac ameipongeza Serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuvutia uwekezaji, kuboresha huduma za afya, sambamba na kupiga vita vitendo vya rushwa.


Ameongeza kuwa, kufuatia jitihada hizo kiwango cha ukuaji uchumi kwa mwaka nchini Tanzania kimefikia asilimia 6.5 na kuwa Tanzania ina mchango mkubwa kwa maendeleo ya Afrika na dunia kwa ujumla. 


Aidha, Mhe. Trac ameahidi kuwa nchi yake itaendelea kushirikiana na kuimarisha uhusiano wake na Tanzania uliodumu kwa takribani miaka 60.


Pia, ameiomba Tanzania kuwa kiunganishi kati ya Vietnam na Umoja wa Afrika katika nyanja mbalimbali za maendeleo.


Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

CPA MAKALLA 'KUUTEKA' MKOA WA ARUSHA

𝗠𝗕𝗢𝗪𝗘 𝗔𝗦𝗜𝗧𝗜𝗦𝗛𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗗𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗬𝗔 𝗖𝗛𝗔𝗗𝗘𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗧𝗔𝗥𝗘𝗛𝗘 𝟮𝟯.

ASKOFU CHANDE AISHUKURU SERIKALI KULIPATIA USAJILI WA KUDUMU KANISA LA KARMELI

DEMU KAMA ANAFANYA KAZI HIZI KUWA MAKINI NAE.

JENGENI UWANJA WA MICHEZO WA KISASA NJOMBE-MWANYIKA