MAMBO YAMEIVA TAMASHA LA WANYAKYUSA DAR


 TAMASHA la Utamaduni wa Mtanzania Jamii ya Wanyakyusa, linatarajiwa kuanza Septemba 27 hadi 29, 2024 katika eneo la Kijiji Cha Makumbusho Kijitonyama Jijini Dar es salaam, lengo likiwa ni kuwakutanisha watu mbalimbali hususani wa jamii ya kinyakyusa pamoja na kuona na kujifunza mila na tamaduni za mnyakyusa.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya, Patrick Mwalunenge, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi siku ya ufunguzi wa tamasha hilo, ambalo litafanyika kwa muda huo wa siku tatu, likitarajiwa kuhudhuliwa na watu zaidi ya 5000, kutoka ndani na nje ya Dar es Salaam.

Ambapo watu hao watapata fursa ya kujionea vitu mbalimbali vya asili ya jamii ya wanyakyusa ikiwa pamoja na Ngoma maarufu kama ‘ Mang’oma, muziki, vyakula vya asili, vinywaji ikiwemo pombe aina ya Kimpumu, Komoni, Kyindi na nyumba zinazoakisi uhalisia wa jamii ya watu wa Mkoa wa Mbeya.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Enelyn Mwakapila, amewaomba wananchi wote hususani wa jamii ya kinyakyusa kujitokeza kwa wingi kuhudhuria katika tamasha hilo, akisema kuwa kufanya hivyo kunakuza hadhi na kuheshimisha tamaduni za makabila ya Tanzania.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

CPA MAKALLA 'KUUTEKA' MKOA WA ARUSHA

𝗠𝗕𝗢𝗪𝗘 𝗔𝗦𝗜𝗧𝗜𝗦𝗛𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗗𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗬𝗔 𝗖𝗛𝗔𝗗𝗘𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗧𝗔𝗥𝗘𝗛𝗘 𝟮𝟯.

DEMU KAMA ANAFANYA KAZI HIZI KUWA MAKINI NAE.

JENGENI UWANJA WA MICHEZO WA KISASA NJOMBE-MWANYIKA

KAMATI YA UWT KUTOA MSAADA WA KISHERIA NCHINI