Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mohamed Mchengerwa wakifunua pazia jiwe la msingi ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, leo tarehe 25 Septemba 2024, ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa ziara yake katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Ruvuma.
Rais Samia akikata utepe wakati wa uzinduzi wa jengo hilo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa eneo la Kigonsera, Wilaya ya Mbinga, baada ya kuzindua jengo la Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, leo tarehe 25 Septemba 2024, ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa ziara yake katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Ruvuma.
Muonekano wa jengo lililozinduliwa.
Wananchi wakiwa na furaha.
Sehemu ya umati wa wananchi ulihudhuria uzinduzi huo.
Comments