RAIS SAMIA AJIONEA USAFIRISHAJI NA UPIMAJI WA MAHINDI RUVUMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 25 Septemba 2024, alipata maelezo kuhusu usafishaji na upimaji wa mahindi unaofanywa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) katika kituo cha ununuzi wa mahindi kilichoko eneo la Soko Kuu, Mbinga mjini, kabla ya kuwasalimu na kuzungumza na wananchi wengi waliokusanyika kumlaki na kumsikiliza.


Kutokana na maelekezo ya Mheshimiwa Rais Samia, katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020 - 2025, NFRA imeweka vituo kwa ajili ya kununulia mahindi ya wakulima katika maeneo mbalimbali nchini, hususan katika mikoa inayozalisha mazao hayo kwa wingi. Hatua hii, mbali na kuwahakikishia wakulima soko la uhakika la mahindi yao na kuwapunguzia adha ya kuyasafirisha umbali mrefu, pia inawalinda dhidi ya ulanguzi wa wafanyabiashara wasiokuwa waaminifu. Aidha, ni mojawapo ya mipango ya Serikali kuweka utaratibu mzuri wa kuyafikisha mahindi hayo katika soko la kimataifa kwa ajili ya manufaa ya wakulima na taifa kwa ujumla.







 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

CPA MAKALLA 'KUUTEKA' MKOA WA ARUSHA

𝗠𝗕𝗢𝗪𝗘 𝗔𝗦𝗜𝗧𝗜𝗦𝗛𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗗𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗬𝗔 𝗖𝗛𝗔𝗗𝗘𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗧𝗔𝗥𝗘𝗛𝗘 𝟮𝟯.

JENGENI UWANJA WA MICHEZO WA KISASA NJOMBE-MWANYIKA

DEMU KAMA ANAFANYA KAZI HIZI KUWA MAKINI NAE.

KAMATI YA UWT KUTOA MSAADA WA KISHERIA NCHINI