ZIARA YA MTOTO WA MALKIA WA UINGEREZA NCHINI

Rais Jakaya Kikwete akiwa na Mtoto wa Malkia wa Uingereza, Prince Charles aliyewasili Ikulu, jijini Dar es Salaam . (PICHA YA IKULU)
JK akiwa na Prince Charles Ikulu leo
Askari wa Usalama wa Taifa, akimuongoza mbwa kunusa sehemu ambayo wanahabari walipangiwa kusimama wakati wa mapokezi ya Prince Charles, Uwanja wa Ndege, Dar es Salaam . Mbwa huyo ni maalumu kwa ajili kutambua vitu vya hatari.(PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
Mama Salma Kikwete akimkaribisha mke wa Prince Charles, Camilla katika ofisi za WAMA
Anuani za makazi zitakavyokuwa zitakuwa zikionesha jina la mtaa, namba ya nyumba na box
Mtoto wa Malkia wa Uingereza, Prince Charles (wa pili kushoto) na mkewe, Camilla (kushoto) wakiangalia albamu yenye stempu za kumbukumbu mbalimbali tangu wakati wa Uhuru mpaka sasa, alipofika kuzindua mpango wa anuani za makazi katika Viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa.
Mke wa Mtoto wa Malkia, wa Uingereza, Prince Charles, Camilla (kushoto) akisalimiana na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kilakala ya Morogoro, alipowasili Ofisi za Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Dar es Salaam. Kulia ni mkabidhi Mwenyekiti WAMA, Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete.(PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
Prince Charles na Mkewe wakinagalia ngoma ya msondo iliyokuwa ikitumbuizwa na kikundi cha JKT
Rubani wa ndege iliyomleta Prince Cherles akiangalia nje walipowasili Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Ndege iliyomleta Mtoto wa Malkia ikiwasili kwenye Uwanja wa Ndege, Dar es Salaam jana
JKT wakitumbuiza kwa ngoma ya Kiborogwe ya wenyeji wa Mkoa wa Mara
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda (kushoto) akizungumza na Mtoto wa Malkia wa Uingereza, Prince Charles aliyewasi alipowasili jana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam. Kulia ni Mke wa Charles, Camila.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.