MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHITIMISHA MBIO ZA UHURU (UHURU MARATHON) KWENYE VIWANJA VYA LEADERS CLUB, KINONDONI, DAR

 Mshindi wa Kwanza wa Mbio ndefu za KM 42 katika Mashindano ya Uhuru Marathon,Jamin Ikai (kutoka nchini Kenya) akiwasili kwenye viwanja vya Leaders Club wakati akimaliza mbio hizo,zilizofanyika leo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania.
 Washindi wa Mbio ndefu za KM 42 katika Mashindano ya Uhuru Marathon wakiwa wamesimama mbele ya mgeni rasmi,mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao.Mshindi wa Kwanza ni Jamin Ikai (kutoka Kenya),Steven Selevestor (kutoka Jeshi la Magereza Tanzania) pamoja na Aley Sanka (Tanzania).
 Washindi wa Mbio ndefu za KM 42 (wanawake) wakiwa wakiwa wamesimama mbele ya mgeni rasmi,mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao.Mshindi wa wa Kwanza ni Thabita Kibet (kutoka Kenya),Naum Jerkosgei (Kenya) pamoja na Banoela Brigton.
 Mgeni Rasmi katika Maadhimisho ya Mbio za Uhuru Marathon,Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa hotuba yake wakati wa maadhimisho mbio hizo zilizofanyika leo kwenye viwanja vya Leaders Club,Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo,ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania. 
 Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Dkt. Fenella Mukangara akisoma hotuba yake kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi,wakati wa maadhimisho mbio hizo zilizofanyika leo kwenye viwanja vya Leaders Club,Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo,ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MUSTAFA MKULO AFARIKI DUNIA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

YANGA BADO POINTI 2 TU ITANGAZE UBINGWA

MAKALLA ASHANGILIWA BUNGENI

DKT NCHIMBI AKARIBISHWA KIMILA NYUMBANI RUVUMA

DKT NCHIMBI AZURU KABURI LA JOHN KOMBA LITUHI, NYASA

MWANACHADEMA MSEMAJI WA WAMACHINGA TAIFA AHAMIA CCM