Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika cha Akiba na Uwekezaji -SAICOS (KIJAICOS), Rwihula Daniel (katikati) akiongoza mkutano mkuu wa ushirika huo, leo kwenye Hoteli ya Lamada, Ilala, Dar es Salaam. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti , Nasra Mohamed na Adam Ngamange ambaye ni Mjumbe wa Bodi. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA
Na Richard Mwaikenda,Ilala
CHAMA cha Ushirika cha Akiba na Uwekezaji (KIJAICOS) kimeunda kamati maalumu ya kutafuta fursa za uwekezaji ili kuuboresha ushirika huo.
Kamati hiyo ya watu sita imeundwa leo wakati wa mkutano Mkuu wa Kijaicos uliofanyika katika Hoteli ya Lamanda, Ilala, Dar es Salaam.
Waliochaguliwa kuunda kamati hiyo ni; Mwenyekiti wa Kijaicos, Rwihula Daniel, Neema Ngowi, Rihard Mwaikenda,Pascal Njereka, Mwalimu Abdallah na Mishomari.
Wametakiwa kufanya utafiti wa miradi inayofaa kwa Kijaicos kuwekeza na kupata faida ili faida inayopatikana wafaidike nayo wanahisa wa Saicos kwa kupata gawio.
Hivi karibuni Kijaicos iliwekeza sh. 362,000 mizinga 10 kwenye mradi nyuki unaoendeshwa na Taasisi ya Maisha Bora Human Development Centre. Hadi sasa mradi huo umeingiza sh. 1,500,000.
Mwenyekiti ameauambia mkutano kuwa Kijaicos iliwekeza pia UTT SH. 500,000 na kupata faida sh. 60,000, Kukamua mafuta ya mchaichai waliwekeza sh. 1,100,000 yaliuzwa mafuta na kupata sh. 900,000 hivyo kuingia hasara ya 200,000.
Mwenyekiti alitaja changamoto zinazoikabili Kijaicos kuwa ni kukosa watendaji wa kutosha na wenye ujuzi, kukosa fedha za kuwekeza katika miradi mikubwa, kukosa ushirikiano wa kutosha kutoka kwa baadhi ya wanachama.
Mwenyekiti Daniel, aliwasome wanachama taarifa ya fedha ambapo viingilio vya wanachama 73 imefikia sh.3,650,000, Michango ya Hisa sh. 3,170,000 na malipo ya kila mwezi ni sh.5,505,000.
Mwenyekiti aliwaomba wanachama kuendele kununua hisa na kuchangia ada za kila mwezi ili kuifanya Kijaicos kuwa hai na kuendelea na mipango mikubwa ya uwekezaji itakayotoa faida kubwa.
Daniel akifafanua jambo katika mkutano huo. Kutoka kulia ni wajumbe wa Bodi ya Kijaicos, Stellah Ngulukulu,Sylvester Kapya, Abdalah Mlangwa na Ngamange
Baadhi ya wanachama wakiwa kwenye mkutano
Wajumbe wakisikiliza kwa makini maendeleo ya mkutano
Mwanachama wa Kijaicos, Pascal Njereka akichangia hoja
Mjumbe wa Bodi ya Kijaicos, Adam Ngamange akifafanua baadhi ya hoja
Mwanachama Hawa Bedui akichangia moja ya hoja za mkutano huo
Mwanachama wa Kijaicos, Rehema Ally akichangia hoja wakati wa mkutano huo. Kutoka kushoto ni wanachama Neema Ngowi, Hawa Bedui.
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 0715264202
Na Richard Mwaikenda,Ilala
CHAMA cha Ushirika cha Akiba na Uwekezaji (KIJAICOS) kimeunda kamati maalumu ya kutafuta fursa za uwekezaji ili kuuboresha ushirika huo.
Kamati hiyo ya watu sita imeundwa leo wakati wa mkutano Mkuu wa Kijaicos uliofanyika katika Hoteli ya Lamanda, Ilala, Dar es Salaam.
Waliochaguliwa kuunda kamati hiyo ni; Mwenyekiti wa Kijaicos, Rwihula Daniel, Neema Ngowi, Rihard Mwaikenda,Pascal Njereka, Mwalimu Abdallah na Mishomari.
Wametakiwa kufanya utafiti wa miradi inayofaa kwa Kijaicos kuwekeza na kupata faida ili faida inayopatikana wafaidike nayo wanahisa wa Saicos kwa kupata gawio.
Hivi karibuni Kijaicos iliwekeza sh. 362,000 mizinga 10 kwenye mradi nyuki unaoendeshwa na Taasisi ya Maisha Bora Human Development Centre. Hadi sasa mradi huo umeingiza sh. 1,500,000.
Mwenyekiti ameauambia mkutano kuwa Kijaicos iliwekeza pia UTT SH. 500,000 na kupata faida sh. 60,000, Kukamua mafuta ya mchaichai waliwekeza sh. 1,100,000 yaliuzwa mafuta na kupata sh. 900,000 hivyo kuingia hasara ya 200,000.
Mwenyekiti alitaja changamoto zinazoikabili Kijaicos kuwa ni kukosa watendaji wa kutosha na wenye ujuzi, kukosa fedha za kuwekeza katika miradi mikubwa, kukosa ushirikiano wa kutosha kutoka kwa baadhi ya wanachama.
Mwenyekiti Daniel, aliwasome wanachama taarifa ya fedha ambapo viingilio vya wanachama 73 imefikia sh.3,650,000, Michango ya Hisa sh. 3,170,000 na malipo ya kila mwezi ni sh.5,505,000.
Mwenyekiti aliwaomba wanachama kuendele kununua hisa na kuchangia ada za kila mwezi ili kuifanya Kijaicos kuwa hai na kuendelea na mipango mikubwa ya uwekezaji itakayotoa faida kubwa.
Daniel akifafanua jambo katika mkutano huo. Kutoka kulia ni wajumbe wa Bodi ya Kijaicos, Stellah Ngulukulu,Sylvester Kapya, Abdalah Mlangwa na Ngamange
Baadhi ya wanachama wakiwa kwenye mkutano
Wajumbe wakisikiliza kwa makini maendeleo ya mkutano
Mwanachama wa Kijaicos, Pascal Njereka akichangia hoja
Mjumbe wa Bodi ya Kijaicos, Adam Ngamange akifafanua baadhi ya hoja
Mwanachama Hawa Bedui akichangia moja ya hoja za mkutano huo
Mwanachama wa Kijaicos, Rehema Ally akichangia hoja wakati wa mkutano huo. Kutoka kushoto ni wanachama Neema Ngowi, Hawa Bedui.
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 0715264202
Comments