Golikipa wa Klabu ya Young Africans Djigui Diarra (Mali) ndiye golikipa pekee ambaye hakuruhusu bao lolote kwenye pumziko hili la kimataifa lililoisha jana. Mali walicheza dhidi ya Guinea Bissau michezo miwili ambapo walipata sare tasa moja na Mchezo mmoja walishinda kwa Goli moja.
Mousa Camara (Guinea) yeye alicheza michezo yote miwili na ana aliruhusu goli moja pekee nyumbani wakati wakicheza na Timu ya taifa la Ethiopia na Guinea walishinda michezo hiyo na kukusanya alama 6.
Ally Salim (Tanzania) alicheza michezo miwili dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na aliruhusu Jumla ya magoli matatu na michezo yote Tanzania ilipotezaa.
NB: Hawa wote wanacheza Ligi kuu ya NBC na 19th October watakuwa kwenye timu zao kwaajili ya mchezo wa derby ya Kariokoo. #NestoShayoUPDATES
Comments