NI MAKOSA WANAFUNZI KUFIKA SHULE SAA 1:15 ASUBUHI

Wizara ya Elimu imewakumbusha waendesha shule nchini kuzingatia sheria inayowataka wanafunzi kufika shule saa 2:00 asubuhi (8:00 AM), huku ikisisitiza kuwa hakuna shule inayoruhusiwa kuwalazimisha wanafunzi kufika mapema zaidi ya muda huo.

Kwa mujibu wa Kanuni 84 ya Sheria ya Elimu ya Msingi ya 2015, saa 2:00 asubuhi ndio muda uliopangwa wa wanafunzi kuanza shughuli zao za shule, huku muda wa saa 1:15 asubuhi (7:15 AM) ukiwa ni muda wa mapema zaidi unaoruhusiwa kwa ajili ya maandalizi kabla ya masomo kuanza na sio chini ya hapo.

Wizara imeonya kuwa itachukua hatua kali dhidi ya shule zitakazobainika kukiuka sheria hiyo kwa kuwalazimisha wanafunzi kufika mapema sana, huku ikisisitiza kuwa muda huo umewekwa ili kulinda afya na ustawi wa wanafunzi na kuhakikisha wanapata usingizi wa kutosha usiku.


 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

OWM–TAMISEMI YASHINDA TUZO YA MABADILIKO YA KIDIJITALI KATIKA TEHAMA AWARDS 2026

VIONGOZI NA WATENDAJI WA MATAWI UVCCM PANGANI WANOLEWA

NMB YAWAUNGANISHA WANANCHI NA HUDUMA, FURSA ZANZIBAR

HIZI HAPA TAKWIMU ZA PETER SHALULILE MCHEZAJI MPYA WA YANGA SC 🔰 🔥

KAMATI YA BUNGE PAC YABAINI MATUMIZI MABAYA YA FEDHA ZA UMMA MZUMBE