"Mimi kwangu Mamelodi Sundown ndio timu pinzani zaidi kwenye mashindano ya CAF na tulipata taarifa kuwa walikuja na scout wao kutazama mchezo wetu dhidi ya Al Ahly pale Cairo"
"Mipango yetu kwa sasa ni kujenga thamani kubwa zaidi Barani Afrika.mwaka Jana tumecheza fainali ya Kombe la Shirikisho ,Mwaka huu tutacheza robo fainali dhidi ya Mamelodi,kwetu hii ni kipimo kikubwa"
"Licha ya ukubwa wa Mamelodi kuwa timu kubwa ,tumejipanga tayari Kwa ajili ya kupambana na Mamelodi Sundown.Niwaombe Wananchi wajitokeze Kwa wingi kuisapoti Yanga maana tunaenda kuweka historia ya kufuzu hatua ya nusu fainali lakini haiwezi Kwa kuwa rahisi lazima ucheze dhidi ya timu nzuri"
"Hatujafika level ya juu lakini walau tumepiga hatua ,Mamelod wametuzudi pakubwa lakini dakika 90 za nyumbani na ugenini zinatosha kuonyesha timu ambayo itafuzu"
Hersi Said (Rais wa Yanga) akieleza kuelekea mchezo wao dhidi ya Mamelod Sundowns kwenye ligi ya Mabingwa Barani Afrika.
Follow Rahma Abdullrazack
#teamofcitizens
Comments