BALOZI NCHIMBI MSIBANI KWA TIXON NZUNDA


KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi amejumuika pamoja na waombolezaji wengine, kutoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Tixon Nzunda, shughuli iliyofanyika nyumbani kwa marehemu, Goba jijini Dar Es Salaam. 


Balozi Dk Nchimbi, ambaye alisoma pamoja na marehemu Nzunda Chuo Kikuu Mzumbe, pia aliwapatia pole familia ya marehemu kwa msiba huo, baada ya kusaini kitabu cha maombolezo.


Mwili wa marehemu Nzunda, ambaye alifariki kwa ajali ya gari Juni 18, 2024 huko wilayani Hai, unatarajiwa kuzikwa nyumbani kwao, mkoani Songwe, Juni 22, 2024.









 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

𝗠𝗕𝗢𝗪𝗘 𝗔𝗦𝗜𝗧𝗜𝗦𝗛𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗗𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗬𝗔 𝗖𝗛𝗔𝗗𝗘𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗧𝗔𝗥𝗘𝗛𝗘 𝟮𝟯.

DEMU KAMA ANAFANYA KAZI HIZI KUWA MAKINI NAE.

KAMATI YA UWT KUTOA MSAADA WA KISHERIA NCHINI

KIKOSI CHA CBE KIMEWASILI ZENJI KUVAANA NA YANGA

YANGA YAWASILI SALAMA ETHIOPIA