Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi leo ameshiriki kikao cha kawaida cha Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) na mafunzo kwa Wajumbe wa Baraza Kuu. Kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Komredi Mohammed Ali Mohammed (Kawaida), kimefanyika katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), jijini Dodoma, leo Septemba 17, 2024.
CPA MAKALLA 'KUUTEKA' MKOA WA ARUSHA
KATIBU wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, CPA Amos Makalla anatarajia kuanza ziara ya siku nne katika Mkoa wa Arusha kuanzia Septemba 4 hadi 7 mwaka huu. CPA Makalla atawasili mkoani humo Septemba 4, ambapo kama ratiba Inavyoonesha atafanya mikutano mikubwa ya hadhara katika Wilaya za Longido, Ngorongoro, Karatu na Monduli. Pamoja na mambo mengine atakayoyafanya katika ziara hiyo, CPA Makalla atakagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025, kuhuisha uhai wa chama, kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kuhamasisha wananchi kujitokeza kuhakiki taarifa zao na kujiandikisha katika Kitabu cha Kudumu cha Wapiga kura, kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba mwaka huu.
Comments