Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, Viongozi walioteuliwa ni kama ifuatavyo:-
(i)
Bi. Nenelwa Mwihambi
ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Kabla ya uteuzi huu, Bi.
Mwihambi alikuwa Katibu wa Bunge; na
(i)
Bw. Baraka Ildephonce
Leonard ameteuliwa kuwa Katibu wa Bunge. Bw. Leonard anachukua nafasi ya Bi.
Mwihambi ambaye ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.
Viongozi
walioteuliwa wataapishwa tarehe 19 Septemba, 2024 saa 09.00 alasiri, Ikulu –
Dar es Salaam.
Comments