HAFLA YA JAMBO LEO KUMUAGA BONIFACE WAMBURA

Mhariri Mkuu wa Jambo Leo, Boniface Wambura (wa pili kushoto),ambaye ameteuliwa kuwa Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), akikabidhiwa zawadi ya kompyuta ndogo iliyotolewa na uongozi wa Kampuni ya Jambo Concepts Tanzania Limited (JCTL), wakati wa hafla ya kumuaga Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa JCTL, Juma Pinto, Meneja Mkuu, Ramadhani Kibanike, Mkurugenzi, Benny Kisaka na  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Perfect Solutions, Evance Aveva ambaye ni Mshauri wa JCTL.

Wafanyakazi wa Kampuni ya Jambo Concepts Tanzania Limited (JCTL), inayochapisha gazeti la Jambo Leo na Jarida la Jambo Brand Tanzania, wakigongeana vinywaji na Mhariri Mkuu wa gazeti  hilo, Boniface Wambura (katikati) kumtakia heri katika kazi yake mpya ya Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), anayoianza kesho.
Hafla hiyo ya kumuaga ilifanyika chumba cha habari cha gazeti hilo, Dar es Salaam

Mkurugenzi Mkuu wa JCTL, Juma Pinto akitoa nasaha
wakati wa hafla hiyo.

Mwandishi wa habari wa gazeti la Jambo Leo, Said Mwishehe akielezea jinsi anavyomfahamu kwa
utendaji kazi, Wambura.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MUSTAFA MKULO AFARIKI DUNIA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

MAKALLA ASHANGILIWA BUNGENI

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI

BASHASHA LATAWALA NCHIMBI ALIPOLAKIWA NA CHONGOLO SONGWE

NCHIMBI AFUNGUA KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA KUMBUKIZI YA MWALIMU NYERERE

DKT NCHIMBI AKARIBISHWA KIMILA NYUMBANI RUVUMA