|
Mhariri Mkuu wa Jambo Leo, Boniface Wambura (wa pili kushoto),ambaye ameteuliwa kuwa Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), akikabidhiwa zawadi ya kompyuta ndogo iliyotolewa na uongozi wa Kampuni ya Jambo Concepts Tanzania Limited (JCTL), wakati wa hafla ya kumuaga Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa JCTL, Juma Pinto, Meneja Mkuu, Ramadhani Kibanike, Mkurugenzi, Benny Kisaka na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Perfect Solutions, Evance Aveva ambaye ni Mshauri wa JCTL. |
|
Wafanyakazi wa Kampuni ya Jambo Concepts Tanzania Limited (JCTL), inayochapisha gazeti la Jambo Leo na Jarida la Jambo Brand Tanzania, wakigongeana vinywaji na Mhariri Mkuu wa gazeti hilo, Boniface Wambura (katikati) kumtakia heri katika kazi yake mpya ya Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), anayoianza kesho.
Hafla hiyo ya kumuaga ilifanyika chumba cha habari cha gazeti hilo, Dar es Salaam |
|
Mkurugenzi Mkuu wa JCTL, Juma Pinto akitoa nasaha
wakati wa hafla hiyo. |
Mwandishi wa habari wa gazeti la Jambo Leo, Said Mwishehe akielezea jinsi anavyomfahamu kwa
utendaji kazi, Wambura.
Comments