James Magai wa gazeti la Mwananchi HATIMAYE Serikali imesalimu amri kwa kukubali kulipa fidia ya Sh 185 bilioni kwa kampuni ya kufua umeme wa dharua ya Dowans Tanzania Ltd, huku Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema akisema kuwa "mjadala kuhusu suala Ulipaji wa fidia hiyo unafuatia uamuzi uliotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Biashara ( "Jopo la wasuluhishi limeamuru zaidi ya Sh36bilioni (dola za Marekani 24,168,343) na riba ya asilimia 7.5 kwa mwaka inayofikia kiasi cha zaidi ya Sh 26bilioni (dola za Marekani 19,995,626) tangu Juni 15, 2010 hadi fidia hiyo itakapolipwa,’ ilieleza sehemu ya uamuzi huo. Pia jopo Jopo "Tanesco wanatakiwa kumlipa mdai (mlalamikaji) Sh3bilioni (dola 1,708, 521) ikiwa ni gharama za uendeshaji wa kesi na gharama zingine na kwamba madai mengine yaliyotolewa na pande zote katika kesi hiyo yanatupwa. Awali baada ya uamuzi huo kufikiwa, Tanesco ilionyesha nia kwamba ingechukua hatua za kukata rufaa, lakini Jaji Werema aliliambia Mwananchi jana katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam kuwa hakuna haja ya suala hilo kukatiwa rufaa, hivyo kuyeyusha ndoto hizo za Tanesco. Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, William Mhando katika mkutano wake na wahariri wa vyombo vya habari wiki mbili zilizopita alisema shirika Hata hivyo, kutokana na kauli ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, sasa ni rasmi kwamba hakutakuwa na hatua zozote za kisheria dhidi ya uamuzi wa ICC na badala yake Tanesco watatakiwa kujipanga kuwalipa Dowans mabilioni hayo ya shilingi Taarifa za ndani ya Tanesco, zinasema kwamba shirika hilo limeanza kuweka fedha kwa ajili ya malipo katika benki moja (jina tunalihifadhi kwa sasa) jijini Dar es Salaam Akizungumza na Mwananchi baada ya hafla ya kuapishwa kwa Jaji Mkuu mpya, Mohamed Chande Othman jana, Jaji Werema alisema ameshamaliza kuisoma hukumu hiyo na kufanya uamuzi ambao tayari ameukabidhi kwa Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja kwa ajili ya hatua nyingine baada ya kuridhika nayo. “Mimi Alisema kwa maana hiyo, haoni haja ya kukata rufaa na kwamba licha ya kusikia baadhi ya watu wakijigamba kwamba wakipewa kesi hiyo wanaweza kushinda, amewaambia mawakili wa serikali kwamba asingependa kusikia uwepo wa mpango wowote wa kukodi mawakili kwa lengo la kuendelea na kesi hiyo. “Kwa hukumu hii siwezi kusema tutalivalia njuga suala la Dowans maana kwa hukumu hii hata ukiivalia hiyo njuga itafikia mahalai njuga hizo zitakatika tu,” alisisitiza Jaji Werema. Kauli ya Jaji Werema imekuja wakati wanaharakati, wananchi wa kawaida na baadhi ya viongozi wa serikali wakipinga waziwazi hukumu hiyo akiwemo Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta aliyekaririwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema kuwa kuilipa fidia Dowans "ni kuhujumu uchumi wa nchi". Sitta ambaye alikuwa Spika wa Bunge la Hata hivyo, katika mazungumzo yake jana, Jaji Werema alisema kwa mtu yeyote makini hawezi kupinga hukumu hiyo kwani mfumo wa uamuzi unaotumiwa na ICC hauwezi kutoa fursa ya kuwepo chochote cha kupinga. Alisema wakati wa usikilizwaji wa kesi hiyo pande zote, yaani Tanesco na Dowans walimchagua msuluhishi wake na kwamba baada ya wasuluhishi hao kutoa uamuzi, ulipelekwa katika mahakama hiyo kwa ajili ya kuupitia na kuuthibisha. Kuhusu hoja kwamba huenda upande mmoja ulitumia mbinu chafu katika kupata ushindi, Jaji Werema alisema msuluhishi anayeteuliwa na pande zinazohusika katika kesi si wakili wa upande wowote na kwamba jukumu “Hata unapomteua mtu kuwa ‘Arbitrator’ (msuluhisi) si wakili wako, hivyo unaweza kumkataa. Kuna taratibu za kumkaba, lakini huwezi kumkataa kwa sababu hafuati mambo yako bali “ Mwanasheria huyo Mkuu wa Serikali alieleza kushangazwa na kejeli na malalamiko yanayotolewa na watu mbalimbali juu ya uamuzi huo akidai kuwa hao wanaopiga kelele sasa wakipinga uamuzi huo ndio baadhi Jaji huyo alisema kuwa kuna upotoshaji katika hukumu hiyo akidai kuwa kuna mambo mengine ambayo yamekuwa yakisemwa katika hukumu hiyo jinsi isivyo sahihi. “Watu wamezungumza Ingawa hakuweza kuainisha aina ya upotoshaji huo, lakini Jaji huyo alisema kwa mujibu wa rekodi, Dowans ilisajiliwa Hivyo alitoa wito kwa Watanzania wote wanaoweza wausome kwanza uamuzi huo ili kuweza kujua hasa mfumo uliotumika katika usuluhishi, hadi kufikiwa kwa uamuzi wa Dowans kupewa haki ya kulipwa. Tanesco inabeba mzigo wa kulipa gharama hizo wakati ambao nchi imekumbwa na mgawo wa umme untokana na kasoro mbalimbali katika mitambo ya kuzalishia nishati hiyo, sambamba na uamuzi wa kupandishwa kwa gharama za umeme ambao umelalamikiwa na wananchi. |
MUSTAFA MKULO AFARIKI DUNIA
* Bi Julie Mkulo*Anasikitika kutangaza kifo cha mume wake *Bw.Mustafa Mkulo* kilichotokea Leo *04-05-2024* Katika *hospital ya Muhimbili Dar es salaam* Shughuli zote za mazishi zitakuwa *Msikiti Maamur* *04-05-2024* Maziko yatakuwa jumapili *05-05-2024* Kilosa Morogoro Taarifa zaidi zitatolewa baadae *Inna lillahi wa inna ilayhi rajioon* Pumzika kwa amani Mustafa Haidi Mkulo, Waziri wa zamani wa Fedha na Mbunge wa zamani wa Kilosa.
Comments