Benki ya NMB imenunua na kugawa vitanda, madawati, viti na meza vyenye thamani ya Shilingi milioni 125.2 katika shule 15 za Wilaya ya Arusha na Arumeru. Kati ya shule hizo zilizonufaika, 11 ni za Arusha Jiji ikiwemo shule za msingi Unga Limited waliopewa madawati 150, huku Baraa, Lemara, Sanawari, Elerai na Kijenge kila moja ikipata madawati 100. Shule zingine ni za sekondari ambazo ni Unga Limited, Elerai, Kimaseki, Osunyai na Salei zilizopokea viti na meza 50 kila moja. Katika Wilaya ya Arumeru, shule ya Sekondari Oldadai imekabidhiwa vitanda vya ghorofa (double decker) 33, huku Kiutu na Kiserian zikikabidhiwa viti na meza 60 kila moja, na shule ya msingi Mussa ikipokea madawati 50. Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa hivyo, Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Baraka Ladislaus, alisema msaada huo una thamani ya Shilingi milioni 125.2. “Kwa shule za Arusha Jiji, vifaa vina thamani ya Shilingi milioni 88.2, huku vifaa vilivyotolewa kwa shule za Arumeru vikiwa na thamani ...
Comments