MABASI madogo manne aina ya Rosa ya kampuni ya Mukeshi Travels yaliyokuwa na watu wanaodaiwa ni mamluki wa CHADEMA waliotoka Tarime na Musoma mkoani Mara kwenda kuvuruga uchaguzi Igunga, yakiwa yameegeshwa eneo la Tinde mkoani Shinyanga kwa ajili ya upekuzi wa Polisi leo. Hata hivyo walidai walikuwa wanakwenda kwenye kampeni huku wengine wakidai wanakwenda kuwa mawakala wa chama hicho siku ya uchaguzi. Kwa mujibu wa habari zilizothibitishwa na Msimamizi wa Uchaguzi mawakala waliapishwa jana. Habari tulizozipata hivi punde ni kwamba watu hao waliodaiwa kuwa mamluki ni kwamba si mamluki wameapishwa leo jioni kuwa mawakala wa chama hicho.(Na Mpigapicha Wetu).
MUSTAFA MKULO AFARIKI DUNIA
* Bi Julie Mkulo*Anasikitika kutangaza kifo cha mume wake *Bw.Mustafa Mkulo* kilichotokea Leo *04-05-2024* Katika *hospital ya Muhimbili Dar es salaam* Shughuli zote za mazishi zitakuwa *Msikiti Maamur* *04-05-2024* Maziko yatakuwa jumapili *05-05-2024* Kilosa Morogoro Taarifa zaidi zitatolewa baadae *Inna lillahi wa inna ilayhi rajioon* Pumzika kwa amani Mustafa Haidi Mkulo, Waziri wa zamani wa Fedha na Mbunge wa zamani wa Kilosa.
Comments