
Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga akikata utepe wakati wa hafla ya uzinduzi wa Jengo la Kibiashara la Kijamii la Quality Centre, Barabara ya Nyerere, Dar es Salaam leo, huku akishuhudiwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad (kulia kwake), Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Seif Idd Ali (kushoto kwake) pamoja na mmiliki wa Jengo hilo, Yusuf Manji

Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa Jengo hilo

Mke wa Mwenyekiti wa Kampuni ya Quality Group Limited, Yusuf Manji, Sukeina Manji (kushoto) akimuonesha nguo mke wa Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga, Ida Odinga, alipokuwa akifanya manunuzi ya bidhaa katika maduka yaliyomo ndani ya Jengo la Quality Centre lililozinduliwa

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya JB Hospitality Limited, Justus Baguma (kulia) akimuongoza Mke wa Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga, Ida Odinga (kushoto) aliyetembelea moja kati ya maduka saba ya kampuni hiyo yaliyomo ndani ya Jengo Quality Centre, muda mfupi baada ya kuzinduliwa rasmi na Raila Odinga, Dar es Salaam. Katikati ni mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Seif Idd Ali, Asha Idd.

Raila Odinga akipongezana na Maalim Seif Sharif Hamad

Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga (wa pili kulia), akioneshwa mandhari ya Hoteli ya kisasa ya Savanna VIP Lounge ya Kampuni ya JB Hospitality, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Jengo la Kibiashara la Kijamii la Quality Centre, Barabara ya Nyerere, Dar es Salaam jana. Kulia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad.

Raila Odinga (wa pili kushoto) akiangalia mchezo wa ng'ombe, alipotembelea moja ya maduka katika Jengo la Quality Centre

\Raila Odinga akichezea mpira alioukuta katika duka la Foot Steps lililomo ndani ya jengo hilo.

Comments