BASI LA NEW FORCE LAUA STENDI YA MABASI MBEYA



Basi la New Force likiwa limeharibika vibaya baada ya kugonga nyumba
  Mgahawa uliopo Stendi Kuu ya Mbeya ulioparamiwa na basi hilo. (picha na habari kwa hisani ya blogu ya Mbeya Yetu)


ABIRIA aliyefahamika kwa jina moja la Amina mkazi wa wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya alikufa papo hapo katika ajali iliyotokea juzi usiku  katika Kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani kutokea Mbeya baada  ya basi la New Force kuparamia ukuta wa mgahawa uliopo mkabala na Ofisi za Mabasi ya Kampuni hilo.
Tukio hilo limetokea majira ya saa 5:00 usiku wa Ijumaa ya Januari 20 mwaka huu  katika Kituo hicho cha Mabasi yakitokea mikoa mingine.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kondakta wa basi hilo aliyejulikana kwa jina la Januari Kapinga aliingia ndani ya basi hilo lenye namba za usajili T 853 AVQ aina ya Yutong lililokuwa likitokea Dar es Salaam baada ya abiria wote kushuka ndipo alipolikurupua kwa nguvu na kumshinda hatimaye kuparamia ukuta.

Abiria aliyefariki alikuwa safarini kuelekea masomoni mkoani Tabora na wakati gari likiparamia ukuta wa mgahawa huo alikuwa akipata chakula cha jioni

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi imesema licha ya mmoja huyo kupoteza maisha, lakini watano wamejeruhiwa.

Aidha kondakta wa basi hilo alitoroka na kwenda kusikojulikana na juhudi za Jeshi la Polis kumtafuta zinaendelea na hadi sasa dereva wa basi hilo anashikiliwa na Polisi kwa mahojiano zaidi.

Kwa upande wake Noah Mwakatumbula Mwenyekiti wa Kituo cha Mabasi mkoani Mbeya yaendayo mikoani amewataka madereva waliopewa dhamana ya kuendesha vyombo hivyo na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waache mara moja tabia ya kuacha funguo za vyombo vyao vya usafiri.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA