Meli ya watalii bahari Hindi yavutwa

Meli ya watalii ya Kitaliana iliyokuwa ikipwelea katika bahari ya Hindi ikiwa na zaidi ya watu 1,000 baada ya kupotelewa na umeme imevutwa hadi kisiwa kimoja cha Ushelisheli.

Meli ya uvuvi ya Ufaransa inaivuta meli hiyo Costa Allegra hadi kwenye kisiwa hicho ambako inatazamiwa kuwasili siku ya Jumatano.

Moto uliotokea katika chumba chenye jenereta ya meli hiyo siku ya Jumatatu ulisababisha kupoteza nguvu zote za umeme.

Meli hiyo inatoka shirika moja na ile meli ya Costa Concordia, ambayo ilikwenda mrama nje ya mwambao wa Italia mwezi Januari ambapo watu 32 walipoteza maisha yao.

Mwaandishi wa BBC Katy Watson aliyeko Ushelisheli anasema meli hiyo inavutwa hadi kisiwa cha Desroches , karibu na kisiwa cha Alphonse kusini Magharibi mwa Ushelisheli.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

Wasifu wa Kizza Besigye

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA