Meli ya watalii bahari Hindi yavutwa

Meli ya watalii ya Kitaliana iliyokuwa ikipwelea katika bahari ya Hindi ikiwa na zaidi ya watu 1,000 baada ya kupotelewa na umeme imevutwa hadi kisiwa kimoja cha Ushelisheli.

Meli ya uvuvi ya Ufaransa inaivuta meli hiyo Costa Allegra hadi kwenye kisiwa hicho ambako inatazamiwa kuwasili siku ya Jumatano.

Moto uliotokea katika chumba chenye jenereta ya meli hiyo siku ya Jumatatu ulisababisha kupoteza nguvu zote za umeme.

Meli hiyo inatoka shirika moja na ile meli ya Costa Concordia, ambayo ilikwenda mrama nje ya mwambao wa Italia mwezi Januari ambapo watu 32 walipoteza maisha yao.

Mwaandishi wa BBC Katy Watson aliyeko Ushelisheli anasema meli hiyo inavutwa hadi kisiwa cha Desroches , karibu na kisiwa cha Alphonse kusini Magharibi mwa Ushelisheli.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI