Mama Mchungaji Elizabeth Mboma (53) akionesha vazi la shule lenye staha ili kuwaonya mabinti wanaovaa sare za ajabu shuleni, wakati wa maadhimisho ya siku ya Wanawake Wakristo (WWK) katika Kanisa la TAG Mwenge jijini Dar es Salaam juzi, ambapo maonesho ya mavazi ilikuwa ni sehemu ya maadhimisho hayo. Wengine ni wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Alpha wanaosali katika kanisa hilo. (NA MPIGAPICHA WETU) Mchg. Tumaini Mwanyonga akiangalia keki yenye umbo la Biblia mara baada ya kuzindua maonesho ya bidhaa ya bidhaa za chama cha Wanawake Wakristo (WWK) wa Kanisa la TAG Mwenge jijini Dar es Salaam jana. Wa pili kulia ni Makamu Mwenyekiti wa WWK Mwenge, Bi. Beatrice Simba akitoa maelezo kuhusu keki hiyo.Wanawake Wakristo (WWK) wa Kanisa la TAG Mwenge jijini Dar es Salaam wakiingia kanisani ili kuanza ibada maalum ya kuadhimisha siku yao jana.
Mama Mchg. Patience Mitimingi akiongoza wimbo maalum wakati wa kuadhimisha siku ya Wanawake Wakristo (WWK) katika Kanisa la TAG Mwenge jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Bi. Mariam Wanga akifurahia wimbo huo.
2Akinamama wa TAG Mwenge wakionesha mitindo ya mavazi ya jioni yenye staha ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya Wanawake Wakristo (WWK) katika Kanisa la TAG Mwenge jijini Dar es Salaam jana. PICHA ZOTE NA IRENE BWIRE
Comments