Mbeki asema mapatano yamepatikana Sudan

Mpatanishi wa Umoja wa Afrika, Thabo Mbeki, ametangaza mapatano baina ya Sudan na Sdudan Kusini kuhusu malipo ya mapato ya mafuta baada ya mzozo wa miezi kadhaa, ambao ulikaribia kuingiza mataifa hayo mawili vitani.
Sudan na Sudan KUsini zijmemaliza mzozo kuhusu ada zinazotozwa mafuta
Bwana Mbeki aliwaambia waandishi wa habari katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa, kwamba maswala yote yaliyokuwa yamebaki, sasa yametatuliwa, lakini hakutoa maelezo zaidi.
Sudan na jirani yake hawakusema kitu hadi sasa.
Sudan Kusini ilisitisha usafirishaji wa mafuta kupitia Sudan mwezi wa Januari, kufuatia mzozo kuhusu ada iliyokuwa ikitozwa na serikali ya Khartoum.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

Wasifu wa Kizza Besigye

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA