Skip to main content

MATOKEO YA KIDATO CHA PILI, DARASA LA SABA YATANGAZWA ZANZIBAR

Na Ali Issa na Zahira Bilali-Maelezo Zanzibar    24/01/2013
 
Jumla ya Wanafunzi 11,195 wamechaguliwa kujiungia Kidatu cha Tatu kwa mwaka wa masomo 2013 katika Skuli mbalimbali za Unguja na Pemba ambapo kati yao wasichana ni 6,768 na wavulana  ni 4,427.
 
Aidha Wanafunzi 17,511 wamefaulu kuingia kidato cha kwanza mwaka huu ambapo kati yao Wasichana ni 9,652 na Wavulana 7,859 .
 
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Ali Juma Shamhuna amebainisha hayo leo wakati alipokuwa akitoa tathimini ya matokeo ya mitihani hiyo huko ofisini kwake Mazizini nje kidogo ya Mji wa Zanzibar
 
Amesema kuwa Wanafunzi waliofanya mtihani wa kuingilia Kidato cha Tatu walikuwa 19,679 ambapo kati yao Wasichana walikuwa 11,045 na wavulana 8644 sawa na asilimia 93.6 %.
 
Aidha ameongeza kuwa ufaulu wa kidato cha Tatu umeongezeka kwa asilimia 0.8 ikilinganishwa na mwaka uliopita.
 
Kwa upande wa Mtihani wa Darasa la Saba Waziri Shamhuna amesema jumla ya Wanafunzi waliofanya mtihani huo walikuwa 23,039 kati yao wasichana walikuwa 12,236 na wavulana 10,803.
 
Akielezea Skuli zilizoshika nafasi ya juu kwa matokeo ya Darasa la Saba Waziri Shamhuna amesema ni pamoja na Kizimbani iliyopo Wilaya ya Wete Pemba na Skuli za Wazazi na Mkunazini zote za Wilaya ya Mjini Unguja.
 
Aidha amezitaja Skuli zilizofanya vibaya matokeo ya Darasa la Saba kuwa ni Kojani, Ukunjwi na Makoongwe zote za Kisiwani Pemba.
 
Kwa upande wa Matokeo ya Kidato cha Pili skuli zilizofanya vyema kuliko nyingine ni Mtoni iliyopo Wilaya ya Magharibi Unguja na Skuli za Msuka na Kiuyu zote za Wilaya ya Micheweni Pemba.
 
Akielezea Skuli zilizofanya vibaya mtihani wa Kidato cha Pili Waziri Shamhuna amesema ni Skuli za Mwenge iliyopo Wilaya ya Magharibi na Skuli za Mfuru matonga na Kinyasini zote za Kaskazini A Unguja.
 
Waziri Shamhuna amezitaja pia Skuli ambazo zitalazimika kufungwa kutokana na kupasisha idadi ndogo ya Wanafunzi ambazo ni Bwefum, Umbuji, Uzi, Ubago,Pongwe Pwani, Michanvi,Mtende,Kisiwa Panza,Makongwe na Ndagoni.
 
Ameongeza kuwa jumla ya Kesi za udanganyifu 12 ziliripotiwa kwa wanafunzi wa Kidato cha pili ambapo Wizara imeamua kwafutia matokeo wanafunzi waliohusika na Udanganyifu huo.
 
 
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR 24/01/2013

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA