HIVI NDIVYO MOTO ULIVYODHIBITIWA PPF TOWER.


Kikosi kazi cha zimamoto kutoka makampuni mbalimbali wakiwa kwenye sehemu ya juu ya ghorofa la PPF Tower lililopo Mtaa wa Ohayo (Ohio) eneo la Posta jijini Dar es Salaam baada ya kuwaka motoleo asubuhi, ambao chanzo chake bado hakijafahamika. Hata hivyo sehemu iliyowaka moto ni sehemu yenye mitambo mingi inayotumika kwa shughuli mbalimbali ndani ya jengo hilo.
Timu iliyodhibiti moto ikiendelea kuzima kabisa moto huo

Pichani askari wa kikosi cha uokoaji cha zimamoto wakiingia kwenye chumba chenye mitambo inayoungua kilichopo sehemu ya juu ya ghorofa hiyo kwa zamu kutokana na kuwepo kwa moshi mzito.
Baadhi ya mashuhuda wakiwa nje ya jengo hilo sehemu ya chini ya ghorofa huku shughuli za uzimaji zikiendelea juu ya ghorofa.
Kama kawaida ya matukio mengi yanayotokea jijini Dar es Salaam mashuhuda hawakosi kama unavyoona pichani huku kila mmoja akitaka kushuhudia kinachoendelea.
Kikosi cha zimamoto kikijipanga eneo la nje ya sehemu ya juu ya ghorofa hilo na kuingia kwa zamu sehemu iliyokuwa ikiteketea.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MUSTAFA MKULO AFARIKI DUNIA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

MAKALLA ASHANGILIWA BUNGENI

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI

BASHASHA LATAWALA NCHIMBI ALIPOLAKIWA NA CHONGOLO SONGWE

NCHIMBI AFUNGUA KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA KUMBUKIZI YA MWALIMU NYERERE

DKT NCHIMBI AKARIBISHWA KIMILA NYUMBANI RUVUMA