Kila mtu achinje na kula, mradi asivunje Sheria
Na
Bryceson Mathias
Nianze kwa
kusema hivi Bundi aliyeiandama Imani ya Madhebu yetu kwa lengo tu la kuboresha
maslahi ya mtu aliyeasisi hoja ya kuchinja ili watanzania waingie katika
malumbano, sasa afahamu hoja yake ya uchovu imeshindwa.
Haiingii
akilini kwa mtu anayetegemewa, mwenye nafasi na dhamana kubwa iliyotukukuka, iwe
ki-Imani au Ki-Itikadi, kuibua migogoro ya dini mithili ya David na Mary katika
kitabu cha Kingereza tulivyosoma hapo kale kidogo, walivyogombea Mtoto na
kumvuta mikono hadi ikakatika.
Kwa muda
mrefu nimekuwa nikisikiliza na kusoma malumbano ya kuchinja nikabaini katika
suala la hilo mmoja wetu miongoni mwa pande zinazobishishania uhalali huo;
anavutia kamba upande wakebadala ya kukaa meza moja na kutengeneza
maridhiano.
Kilichopelekea
mgogoro huu hasa, yawezekana kabisa umetokana na kupotoka kwa baadhi ya
dni ambazo pengine zinajiona ni bora kuliko Dini nyingine, huku wakisahau
kujali kwamba wenzao wenye miiko ya dini zao ya kutokula kitoweo kilichochinjwa
au kutochinjwa na dini nyingine.
Kwa mfano;
kwa mila na desturi katika Jamii au familia, kuna watu hawali vitu fulani fulani
kama Njiwa, Kuku, Bata, Nyama, Samaki na vitu vingine katika koo na familia zao.
Hivyo hatupaswi kuwalazimisha au kuwapuuza kwa kile wanachokiamini, na akitokea
mtu wa namna hiyo atakuwa Mkorofi.
Kimsingi
kwa ukweli halisi, Serikali haitakiwi kubabaika kiasi cha kuuma maneno na kukaa
kimya, bali isema wazi kwamba kila mtu anaweza kuchinja kutokana na imani yake
ilimradi tu havunji sheria za nchi kwa maadili yoyote.
Je; mtu
akila Mlenda nyumbani kwake au akaamua kuchinja Kuku, Bata, Njiwa, Mbuzi au
kitoweo chochote alichonato, kuna ulazima wa kumlazimisha achinjiwe? Je tuna
haja ya kumlalamikia na kumtuhumu kiasi cha kumsababishia ghasia na magombano
akiwa ametulia kwake?
Lakini
nakubaliana kwamba, Mfanya Biashara wa Kikristo au Wa K-Islamu, akitaka kufanya
Biashara ya Nyama, Sherehe, Msiba, au kusanyiko lolote linalohusisha Kula, ni
lazima uchinjaji wa kitoweo chake uhusisishe ridhaa ya uchinjaji ambao utaruhusu
Watu wote kwenye kusanyiko hilo kula.
Kwa maana
hiyo viongozi, wananchi na waumini wa madhehebu mbalimbali nchini waelewe
kwamba, Wapagani, Wakristo, Wa-Islamu wanaweza kuchinja kitoweo chao na wakala
endapo wako katika familia zao, kama ilivyokuwa ikifanyika hapo awali bila
kuathiri chochote ili mradi havunji sheria za nchi.
Hivi kama
huli kitu, na wengne wanakula, kwa nini upate uchoyo na uroho wa kutaka kula kwa
tamaa yako? Mimi sioni kitu hapa maana hakuna Mkristo au M-Islam ambaye ni bora
kuliko mtu wa Dini zingine, hiyo inatokana na miiko au mila za dini zao za
kutokula vitoweo vilivyochinjwa na dini nyingine.
Mbona huko
Ulaya, wenzetu wana maduka ya Bucha ambapo Wakristo wana ya kwao wananunua
wanachokita na wa- Islamu wana ya kwao wanunua wanachokita kwa nini sisi
tugombane hata kwa vitu ambavyo hatuvili? ningekuwa mimi, akichinja Mu-Isalmu
nakula; maana najua jinsi ya kufanya ili nile
Hivyo
Usichokula usikionee uroho na tamaa ya kukila, na pia tusiwabeze
wanaokula.
Comments