BALOTELLI AFUNGA MABAO MAWILI AC MILAN IKIUA 4-0 NA KUKATA TIKETI YA KUCHEZA LIGI YA MABINGWA MSIMU UJAO
MTALIANO Mario Balotelli amefunga mabao
mawili usiku huu ikiwemo penalti babu kubwa, akiiwezesha AC Milan kupata
nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuichapa Pescara
mabao 4-0.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa
Manchester City alifunga bao lake la kwanza kwa penalti kabla ya kufunga
lingine katika mechi ambayo wachezaji wengine waliowahi kucheza Ligi
Kuu ya England Sulley Muntari na Mathieu Flamini walifunga.
Amekuwa na mafanikio tangu arejee Italia
na Milan wamekuwa hawafungwi katika mechi ambazo anacheza Serie A,
ikishinda nane na kutoa sare tatu.
Mario Balotelli akifunga kwa mkwaju wa penalti
Balotelli akishangilia na Robinho
Waliocheza England wanatisha: Sulley Muntari akishangilia bao lake
Balotelli akimtoka Marco Capuano
Wachezaji wa Milan wakishangilia
Comments