KIINGILIO SIMBA NA YANGA SH 5,000 'KWA WALALA HOI' NA 30,000 KWA MASHEFA


Yanga Gombani
Na Mahmoud Zubeiry, IMEWEKWA MEI 14, 2013 SAA 7:5 MCHANA
MASHABIKI watakaotaka kwenda kushuhudia mpambano wa mahasimu wa jadi katika soka ya Tanzania, Simba na Yanga SC Jumamosi wiki hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam watalazimika kulipa Sh. 5,000, hicho kikiwa kiingilio cha chini zaidi katika sehemu ya viti vya Rangi ya Bluu. 
Aidha, katika mchezo huo wa kufunga pazia la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, utakaoanza saa 10:00 jioni, viingilio vingine ‘nafuu kidogo’ vitakuwa ni Sh 7,000 kwa viti ya Rangi ya Kijani na Sh. 10,000 kwa viti vya Rangi ya Chungwa.
Upande wa ‘wakubwa’, viingilio vitakuwa ni Sh. 15,000 kwa VIP C, Sh. 20,000 kwa VIP B na Sh. 30,000 kwa VIP A.
Ofisa Haabri wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura amesema kwamba viingilio hivyo ni sawa na viingilio vya mchezo wa mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo baina ya miamba hao, Oktoba 3, mwaka jana. 
Wambura alisema tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo, yaani Ijumaa wiki hii katika vituo mbalimbali vitakavyotajwa.
Simba Mao Dze Tung

Tayari miamba hiyo ya soka nchini iko mafichoni kwa maandalizi ya mpambano huo.
Yanga wameweka kambi yao kisiwani Pemba katika hoteli ya Samail mkabala na benki ya PBZ, wakifanya mazoezi Uwanja wa Gombani wakati Simba wameweka kambi maeneo ya Mbweni JKT Zanzibar wakifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Mao Dze Tung.
Wakati Yanga walitua Pemba Ijumaa jioni, mahasimu wao wa jadi, Simba SC waliwasili Zanzibar Jumapili jioni na mara moja kuanza kujifua kwa ajili mchezo huo, unaosubiriwa kwa hamu.   

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA