Mapenzi ni dhana pana sana. Ni dhana ambayo mpaka hivi leo mwanadamu bado anahangaika kupata ufafanuzi wake. Hata hivi leo tukiuliza hapa hivi mapenzi ni nini,tunaweza kupata maoni zaidi ya hata elfu moja huku kila mmoja akiwa na maana au tafsiri yake kuhusu mapenzi. Usishangae kama tafsiri hiyo yaweza kuwa tofauti kabisa na yako au yangu!
Bahati nzuri au mbaya ni kwamba mwisho wa siku wote tutakuwa sahihi. Kila mmoja anaruhusiwa kutafsiri dhana ya mapenzi au penzi kwa kadri anavyoona yeye au kwa jinsi ambavyo “mvua inakuwa imemnyeshea”.Si unakumbuka kwamba aisifiaye mvua imemnyeshea?
Upana wa dhana ya mapenzi huenda ndio hupelekea kila kukicha wanamuziki wanazidi kutunga na kuimba nyimbo kuhusu mapenzi. Mapenzi hayajaanza jana wala leo na hayatokaa yafikie mwisho.
Pamoja na hayo, zipo nyimbo za mapenzi ambazo wenzetu wanaotumia kizungu huwa wanasema “it has stood the test of time” kumaanisha kwamba wakati sio kitu kwake kwani kitu hicho(nyimbo) bado kinapendwa na kitaendelea kupendwa kwa wakati mwingi ujao.Mfano mzuri wa nyimbo za aina hiyo ni ule uitwao Maria (Mary Maria) ulioimbwa na Vijana Jazz Band enzi hizo ikiwa chini ya uongozi wa Hayati Hemed Maneti(pichani). Katika wimbo huo utamsikia Maneti akilalama kutokana na penzi zito alilonalo kwa “mtoto” Mary. Baadhi ya maneno kwenye wimbo huo ni kama;
Kwa kweli sasa nimenaswa
Sina ujanja eeeh eeeh,
Sina ujanja eehhh
Kupenda sawa na ajali
Haina kinga eeh eeh
Haina kinga eeh
Nilivyomuhusudu mtoto Mary sijapata kupenda toka nizaliweeeee
Na wala sitapenda mpaka nife,
Mpaka nife, mama Mary oooh

Bonyeza player hapo chini upate burudani kamili ya wimbo Maria.Kama unaye umpendaye, huku naye anakupenda kwa dhati na wala sio “for convenience” basi muite mwambie mcheze kidogo wimbo huu.Nakutakia Ijumaa Njema.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI