Warembo wanaogombania Miss Manyara 2014
Warembo wanaogombania Miss Manyara 2014 wakiwa wanacheza mmoja ya wimbo watakaoucheza katika siku ya mashindano ikiwa ni moja ya sehemu ya mazoezi. Picha na Woinde Shizza.
Na Woinde Shizza, Manyara
Kinyanganyiro
cha kugombea Redd's Miss Manyara 2014, kinatarajia kufanyika kesho
Jumamosi Juni 14 mwaka huu katika ukumbi wa CCM Mkoa, mjini Babati,
ambapo warembo 10 wanatarajia kuchuana.
Mkurugenzi
wa Mirerani Entertainment, Akon Clement ambaye ni Mratibu wa mashindano
hayo alisema mgeni rasmi wa mashindano hayo anatarajiwa kuwa Waziri wa
Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Mary Nagu.
Akon
alisema msanii maarufu wa kizazi kipya, Bob Junior kutoka jijini Dar es
salaam anatarajiwa kutoa burudani kali wakati akisindikiza michuano hiyo
ambapo pia wasanii chipukizi kutoka mjini Babati watashiriki
kunogesha.
Aliwataja
wanyange hao wanaotarajia kushiriki mashindano hayo kuwa ni Miss
Mirerani 2014 Amina Omary, Miss Mirerani namba mbili Catherine Emmanuel
na Miss Mirerani namba tatu Happy William.
Wengine
ni Fatuma Salim, Betha Fredrick, Rose Evason, Edna Mushi, Hosiana John,
Mary Ruta na Flora Godlizen, ambao ni warembo walioshinda kwenye
mashindano ya wilaya za Babati, Hanang' na Mbulu, alisema Clement.
Aliwataja
wadhamini wa mashindano hayo ni kampuni ya Tanzania Breweries (TBL),
kupitia kinywaji chake cha Redd's Original, Open University, Manyara
Computer, mireranitanzanite.blogspot.com,libeneke la kaskazini blog na
Active Classic Fashion.
Mratibu
huyo alisema kuwa wadhamini wengine wa shindano hilo ni TanzaniteOne,
Assey Printing company, Trimus Saloon, Kifaru Agrovet, Winners Hotel,
Sarafina Lodge na Kimweri Sport Wear.
Comments