PICHA:NYOKA AINA YA CHATU AUWAWA KANISANI BAADA YA KUKUTWA NYUMBANI KWA MFANYABIASHARA MAARUFU JIJINI ARUSHA AKISADIKIWA KWA IMANI ZA KISHIRIKINA
Joka
hilo kubwa aina ya Chatu likiwa nje ya Nyumba ya mfanyabiashara huyo,
ambalo lilikutwa likiwa limefungwa Kitambaa cheupe kilichokuwa na
maandishi ya Kiarabu, ambapo wananchi wamefananisha suala hilo na imani
za kishirikina. Joka hilo baada ya kudhibitiwa liliburuzwa hadi katika
Kanisa Katoliki la Karsamatiki lililopo eneo la Sakina jijini Arusha na
kuanza kuuawa na wananchi.
Chatu huyo akiburuzwa kuelekea kucharangwa baada ya kuuawa.
Kijana akiwa amembeba nyoka baada ya kucharangwa kwa mapanga akitoka naye nje ya uzio wa kanisa hilo
Nyumba
ya mfanyabiashara maarufu wa jijini Arusha, aliyetambulika kwa jina la
Joseph Magese, alikotolewa nyoka huyo aina ya Chatu na kuuawa na
wananchi kwa kucharangwa mapanga.
Kitambaa chenye maandishi ya kiarabu alichokutwa nacho nyoka huyokikiwa mbele ya geti la nyumba ya mfanyabiashara huyo
umati wa watu waliofika kushudia tukio hilo
Comments