DIWANI VITI MAALUM CCM LUDEWA AFARIKI DUNIA


diwani  wa  viti maalum  Lupingu Prisca Kayombo(Zaruta) . wa  tatu  kulia  akiwa na mbunge wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe kulia na katibu wake Stan Gowele  na wananchi9  wengine wa Ludewa  wakijiandaa kunyanyua nguzo ya  umeme  enzi wa uhaki wake  wiki mbili zilizopita 
 Wananchi  wa Lupingu  Ludewa  wakilitazama  daladala  lililopata  ajali  na kusababisha  kifo cha aliyekuwa  diwani wa viti maalum kata ya  Lupingu Prisca  Kayombo  leo



Diwani wa  viti maalum  Lupingu Prisca Kayombo(Zaruta) akishiriki kubeba  nguzo ya  umeme 



Diwani wa viti maalum Lupingu Prisca Kayombo(Zaruta)  kulia  akishirikiana na mbunge wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe  kufukia  nguzo za umeme  kwenda kata ya Lupingu katika kijiji cha Ntumbati wiki  mbili kabla ya  kifo chake leo 

Gari ya wagonjwa ikiwashusha majeruhi katika Hospitari ya wilaya ya Ludewa waliokuwamo katika ajari
hiyo

 majeruhi wakishushwa hospitari



 Wananchi wa kata ya Ludewa wakishuhudia majeruhi waliokuwa wakishushwa katika gari ili kuwatambua

                               Habari na  picha na   Matukiodaima.co.tz

DIWANi  wa  viti maalum kata ya Lupingu  wilaya ya  Ludewa Prisca Kayombo(Zaruta) amekufa  papo hapo na wengine kujeruhiwa  vibaya katika ajali ya  ajali mbaya ya gari  iliyotokea  leo asubuhi.

Mashuhuda wa  ajali  hiyo  waliozungumza na mtandao  huu  walidai kuwa  chanzo cha ajali  hiyo ni gari hilo ambalo  walikuwa  wakisafiriki  kutoka  Lupingu - Ludewa  kufeli  breki na hivyo  kupinduka .

Credo Haule  alisema kuwa  baada ya  gari hilo aina ya Toyota Costa inayojulikana kwa jina la DMX iliyokuwa ikifanya safari zake kutoka Ludewa Mjini kuelekea Lupingu ,kufeli  breki dereva  aliwataka  abiria  kutulia ndani ya  gari  hilo ila  diwani huyo hakuweza kufanya  hivyo na kuamua  kuchukua maamuzi magumu ya kutaka  kuruka katika gari  hilo.

Alisema  kuwa  wakati akiruka  alimsukuma  utingo wa  basi hilo na hivyo  wote  wawili utingo na diwani  kufunikwa na gari hilo na kupelekea kifo cha  diwani  huyo  huku utingo  huyo akiwa mahututi  baada ya  kubanwa na gari hilo.


" Diwani  huyo amepoteza maisha  wakati akiwa njiani kuelekea  kujumuika na  wananchi wake katika  shughuli ya  maendeleo ya  kuchimba mashimo ya nguzo za umeme  kuelekea kijijini kwake  Lupingu"

Mbunge wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe ameeleza  kusikitishwa na kifo  cha  diwani  huyo  kutokana na mchango  wake mkubwa aliouonyesha  enzi wa uhai  wakati kwa kushiriki  vema na  wananchi wa kata  yake katika zoezi la kufyeka na kuchimba mashimo ya nguzo za umeme kwenda Lupingu.

Alisema  kuwa anakumbuka  ni wiki  mbili  pekee  zimepita  toka diwani  huyo  alipoungana nae katika  uchimbaji wa mashimo ya nguzo za umeme  kwenda kijiji cha Ntumbati na kuwa  hata wakati ajali  hiyo inamkuta  bado  alikuwa katika harakati za kuwatumikia  wananchi  wake.

" Ludewa  tumempoteza  diwani mchapa kazi na aliyependa  kujituma muda  wote na hata  wakati  mwingine diwani  huyo alikuwa akifanya kazi  ngumu kama mwanaume  kwa  kubeba  nguzo za umeme kwa  kushirikiana na mimi na wananchi  wake .....kwweli kifo  chake ni pigo kubwa  ndani ya CCM na kwa  wananchi  wa kata  nzima ya  Lupingu"

Kwani kati ya madiwani  waliokuwa  bega kwa bega na wananchi  wao na mbunge ni pamoja na diwani  huyo ambae  alikuwa mstari wa mbele  kuona kata ya Lupingu inapata  umeme wa uhakika baada ya  miaka zaidi ya 50 ya Uhuru  bila umeme .

Mbunge  Filikunjombe  alisema  atamkumbuka  diwani  huyo kutokana na mchango  wake mkubwa katika maendeleo na vile  alivyofanya kazi na wananchi wote  bila  kujali itikadi zao za vyama.

Mkuu  wa  wilaya ya  Ludewa Juma Madaha  amethibitisha  kutokea kwa  ajali  hiyo  iliyosababisha  kifo cha  diwani  huyo na kuwa ajali hiyo ilitokea majira ya saa 2  asubuhi .

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI