𝗠𝗮𝗸𝗮𝗯𝗶𝗹𝗮 10 𝗮𝗺𝗯𝗮𝘆𝗼 𝘂𝗸𝗶𝗸𝗮𝗮 𝗸𝗮𝗿𝗶𝗯𝘂 𝗻𝗮𝗼, 𝗸𝘂𝘁𝗼𝗯𝗼𝗮 𝗸𝘂𝗻𝗮𝘄𝗲𝘇𝗮 𝗸𝘂𝘄𝗮 𝗿𝗮𝗵𝗶𝘀𝗶 𝘇𝗮𝗶𝗱𝗶 ⚠️ Kumbuka: Haya ni maoni na mitazamo ya kijamii tu, si kwamba kabila fulani lina mafanikio kuliko lingine. Mafanikio yanategemea juhudi, elimu, nidhamu na fursa. 1. Wasukuma Wana sifa ya kufanya kazi kwa bidii, hasa kwenye kilimo, ufugaji na biashara. Wengi huaminika kuwa wavumilivu katika kutafuta maendeleo. 2. Wachagga Hujulikana kwa moyo wa biashara, uwekezaji na kusaidiana kifamilia katika shughuli za maendeleo. 3. Wahaya Wana historia ndefu ya biashara, elimu na shughuli za uzalishaji zinazochochea maendeleo. 4. Wanyakyusa Wengi wanasifiwa kwa bidii katika biashara, kilimo na uwekezaji wa muda mrefu. 5. Wakinga Hujulikana kwa uchapakazi, nidhamu na uthubutu wa kutafuta fursa sehemu mbalimbali za nchi. 6. Waha Wana sifa ya kujituma katika biashara na shughuli mbalimbali za kiuchumi. 7. Wapare Mara nyingi husifiwa kwa kuthamini elimu, kazi na mipango y...
MBUNGE DEO MWANYIKA AFANYA ZIARA YA KIKAZI KATA YA MJI MWEMA, AKAGUA MIRADI NA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI Mbunge wa Jimbo la Njombe, Mhe. Deo Mwanyika, jana tarehe 3 Agosti 2026, alifanya ziara ya kikazi katika Kata ya Mji Mwema kwa lengo la kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo, kuzungumza na wananchi pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili. Katika ziara hiyo, Mhe. Mwanyika alikagua Daraja la Kifung’a, lililopo katika barabara inayounganisha maeneo ya Mji Mwema na Ramadhani. Ukaguzi huo ulimwezesha kujionea hali halisi ya daraja hilo pamoja na umuhimu wake katika kurahisisha usafiri wa watu, mazao na huduma nyingine muhimu. Aidha, Mhe. Mbunge alitembelea na kukagua ujenzi wa nyumba ya mwalimu katika Shule ya Msingi Peluhanda. Alipokea taarifa kuhusu hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo na kusisitiza umuhimu wa kuboresha mazingira ya kuishi na kufanya kazi kwa walimu ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa elimu. Baada ya kukagua miradi hiyo, Mhe. Mwa...
1. Wahiraki, Hawa ni wanawake wa jamii ya Wahiraki wa napatikana kaskazini mwa Tanzania wamezagaa mikoa ya manyara ni weupe Wana Umbo zuri wanavutia kwa Macho. 2. Warangi, Hawa ni wanawake jamii ya Warangi ni wazuri nywele zao ni asili ya waraabu weupe sura nzuri wanapatikana kondoa. 3. Wanyiramba. Hawa ni warembo Sana sura matata wanapatikana mkoa wa singida kaskazini, usipokua makini utawafananisha na wanyaturu 4. Wamasai, kabila hili wanawake wazuri sio wengi Sana lakini ukikutana na sampuli Tatu au nne hivi utauza hata boxa kuongezea mahari wamezagaa Sana Arusha 5. Wahaya, hawa nao ni jamii ya Kanda ya ziwa maumbile Yao Kuna weupe miguu Yao ya bia shape matata wamejaa Sana bukoba. 6. Wanyaturu, Hawa wanafanana na Wanyiramba wanapatikana singida hasa ikungi na manyoni weupe wanavutia 7. Wapare, Hii ni jamii ya kabila la Wapare wanapatikana moshi wilaya ya same wako vizuri usicheze kabisa na hili kabila shape nzuri. 8 .Wamakonde, ...
NA MWANDISHI WETU OFISI ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) imeshinda tuzo ya TEHAMA AWARD 2026, katika kipengele cha Mabadiliko ya Kidijitali katika Sekta ya Umma. Tuzo hizo zilizoandaliwa na Tume ya TEHAMA, zilitolewa Agosti 09, 2026 kwenye hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Johari Rotana, jijini Dar es Salaam. Hafla hiyo ilihudhuriwa na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Kairuki, ambaye alikuwa Mgeni Rasmi. Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) imeibuka mshindi wa kwanza katika kipengele hicho, ikifuatiwa na Shirika la Posta Tanzania (TPC) lililoshika nafasi ya pili, huku Wizara ya Afya ikishika nafasi ya tatu. Mbali na ushindi huo, OWM–TAMISEMI pia ilishika nafasi ya pili katika vipengele mbalimbali, ambavyo ni Utangazaji wa Maudhui ya Kidijitali, Matumizi ya TEHAMA kwa Ajili ya Athari Chanya katika Jamii, Matumizi ya TEHAMA katika Huduma za Afya, pamoja na Ubora katika Akili Mnemb...
Makundi maalumu 27,946 yamesajiliwa kwenye m fumo wa NeST na ku pata zabuni zenye jumla ya thamani ya Shilingi Bilioni 56 , kupitia Mfumo huo. makundi ya vijana ni 13, 317 wanawake 13,400 , wazee 643 na watu wenye ulemavu 586. Hayo yemebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Dennis Simba wakati wa mkutano na vyombo vya habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO, katika Mji wa Serikali wa Mtumba jijini Dodoma, Agosti 20, 2026. Sheria ya Ununuzi wa Umma, imezielekeza taasisi zote za umma kutenga asilimia 30 ya bajeti zao za ununuzi kwa ajili ya makundi maalum (vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu). Lengo la PPRA, kwa kuzingatia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ni kuwa na takribani makundi 300,000 yaliyo tayari kuomba zabuni. Hatua hii ni sehemu ya jitihada za Serikali kutoa ajira na kazi kwa Watanzania ambao hawana uwezo wa kuwa na kampuni, ambao wanaweza kujiunga k...
NA: MWANDISHI WETU, PANGANI Viongozi na watendaji wa matawi wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), wilaya ya Pangani mkoani Tanga, wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa masuala mbalimbali ya kichama, kiuongozi na kijamii ili kuboresha utendajikazi wao wa kila siku. Mafunzo hayo yametolewa Agosti 2, 2026, katika Kata ya Kipumbwi wilayani humo. Akizungumza katika mafunzo hayo, Mwenyekiti wa Seneti ya vyuo vya kati, vyuo na vyuo vikuu mkoa wa Tanga, Leila Mnaki, ambaye alikuwa miongozo mwa wakufunzi, amesema CCM ni Chama imara kwani misingi yake ipo ngazi za chini za mabalozi na matawi, hivyo ni wajibu wa Chama kutoa mafunzo ya mara kwa mara kwa viongozi wake ili kuboresha utendajikazi. "Nguvu ya Chama ni wanachama na viongozi wake, ndiyo maana tupo hapa kupata mafunzo ya kutujengea uwezo ili utendajikazi wetu uwe wenye tija kwa manufaa ya Chama na wananchi tunaowahudumia," amesema Mnaki. Aidha, Mnaki amesema, ni wajibu wa viongozi kuwahudumia wananchi kwa kufuat...
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akikabidhi cheti cha kutambua ushiriki wa NMB katika kufanikisha Tamasha la Kizimkazi 2026 kwa mwakilishi wa benki hiyo. ………… ZANZIBAR. Benki ya NMB imehitimisha ushiriki wake katika Tamasha la Kizimkazi 2026 kwa kuunganisha wananchi na huduma za kifedha pamoja na fursa za kukuza biashara. NMB ilikuwa miongoni mwa wadhamini wa tamasha hilo lililofikia kilele jana, Agosti 14, Kusini Unguja. Banda la benki hiyo lilitumika kutoa elimu ya fedha na kueleza huduma zinazolenga wafanyabiashara, wajasiriamali na wananchi wa Zanzibar. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipotembelea banda hilo, alipokea maelezo kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Biashara za Serikali wa NMB, Vicky Bishubo, kuhusu ushiriki wa benki katika tamasha na huduma ilizopeleka kwa wananchi. Ushiriki huo umeimarisha nafasi ya Kizimkazi kama jukwaa la kutangaza fursa za kiuchumi, kuibua biashara na kuleta huduma muhimu karibu na jamii...
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt, Samia Suluhu Hassan alipotembelea na Kuzindua Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka awamu ya pili (BRT II) Mbagala jijini Dar es Salaam Leo August 07, 2026.
Jina Kamili: Peter Shalulile Tarehe ya Kuzaliwa: Oktoba 23, 1993 Nchi: Namibia Nafasi: Mshambuliaji (Striker) / Nahodha Urefu: Sentimita 174 Mguu wa Kazi: Kulia Historia ya Vilabu Alivyochezea Tura Magic FC (Namibia) – Alianzia hapa soka lake la ushindani. Highlands Park FC (Afrika Kusini) – Alijiunga nayo akitokea Namibia kabla ya kuhamia Mamelodi. Mamelodi Sundowns FC (Afrika Kusini) – Alijiunga Julai 2020 hadi Julai 2026, alipoiacha timu hiyo akiwa amefunga mabao zaidi ya 100. Mafanikio na Rekodi Kuu Mataji ya Ligi: Ametwaa mataji 5 ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini (PSL) akiwa na Mamelodi Sundowns. Ligi ya Mabingwa Afrika: Alisaidia Sundowns kubeba ubingwa wa CAF msimu wa 2025/26. Tuzo Binafsi: Amewahi kuwa Mfungaji Bora wa Ligi Kuu ya Afrika Kusini na Mchezaji Bora wa Msimu mara kadhaa kutokana na ukali wake langoni. Timu ya Taifa: Nahodha na kinara wa kufunga mabao wa muda wote katika kikosi cha timu ya taifa ya Namibia (Brave Warriors
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) haijaridhishwa na maelezo yaliyotolewa na Chuo Kikuu cha Mzumbe kuhusu hoja zilizobainishwa katika Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2024/2025. Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Devotha Minja, amesema Kamati imebaini dosari katika matumizi ya fedha za umma, ikiwemo manunuzi yaliyofanyika bila kuzingatia matakwa ya Sheria ya Manunuzi ya Umma. Akizungumza na waandishi wa habari leo, Agosti 18, 2026, Bungeni jijini Dodoma, Minja amesema PAC haijaridhishwa na majibu ya Chuo kuhusu hoja hizo na kwamba baadhi ya maelezo yaliyotolewa hayajatoa majibu ya kuridhisha kwa Kamati. Kwa mujibu wa Taarifa ya CAG, Chuo hicho kilifanya manunuzi yenye thamani ya Sh bilioni 29.77 kutoka kwa wazabuni ambao hawakukidhi vigezo, huku Sh bilioni 1.54 zikilipwa kwa watu ambao hawakukidhi viwango vilivyowekwa. Aidha, Kamati imeeleza kutoridhishwa na ujenzi wa barabara yenye thamani ya Sh milioni 523, ambayo imeelezwa...
Comments