Rais wa marekani Donald Trump amekutana na Rais wa Ukraine ndugu Volodymyr Zelenskiy pale White House jijini Washington, D.C., February 28, 2025. Mkutano wa Ikulu ya White House kati ya Rais wa Marekani Donald Trump na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy uliolenga kupata makubaliano ambayo yangeruhusu Marekani kupata haki adimu za madini ya Ukrain uligeuka kuwa mechi ya kelele kati ya viongozi hao wawili huku Trump akimtishia Zelenskyy kwa "Utafanya makubaliano au tunatoka." Katika taarifa yake kwenye mitandao ya kijamii kufuatia mkutano huo, Trump alionyesha kuwa makubaliano hayo yamezimwa. "Nimeamua kuwa Rais Zelenskyy hayuko tayari kwa Amani ikiwa Amerika itahusika, kwa sababu anahisi kuhusika kwetu kunampa faida kubwa katika mazungumzo," Trump aliandika. Zelenskiy na Trump wamesuguana kwa hoja na vioja baada ya Zelenskiy kumshutumu Trump kuwa amekuwa laini mno kwa rais wa Russia Vladimir Putin huku Trump akimshutumu zelenskiy kuwa hana...
SERIKALI imesema itajenga Arena yenye uwezo wa kuingiza zaidi ya watu 15,000 katika eneo la Kawe Dar es Salaam. Kauli hiyo inakuja baada ya msanii wa muziki wa kizazi kipya Nassibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kumuomba Rais Samia Suluhu Hassan kuharakisha ujenzi wa Arena ili wasanii wapate ukumbi wa kufanya shughuli zao. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Gerson Msigwa amesema baada ya Rais Samia kufanya ziara Korea, amepata mkopo wa masharti nafuu wa Dola bilioni 2.5. Advertisement “Kati ya fedha hizo ameamua kukata Sh bilioni 450 kwa ajili ya kuzileta Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kujenga Arena kwanza halafu itafuatia kijiji cha filamu,”amesema. Amesema fedha zitakapotoka Korea na kufika kwao wataanza ujenzi wa Arena mara moja ili uwanja huo uanze kutumika kwa ajili ya shughuli za michezo na burudani. “Arena inakuja, ndugu zangu wasanii tumshukuru sana Rais Samia, hili jambo lilikuwa linamu...
WAAMUZI wa Tanzania Ahmed Arajiga, Kassim Mpanga, Said Hamdani na Salum Nasir wameteuliwa na na Shirikisho la soka Duniani (FIFA) kuchezesha mchezo wa Kundi G wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2026 kati ya wenyeji Botswana dhidi ya Algeria utakaopigwa Mjini Francistown Nchini Botswana Machi 21, 2025. Algeria na Msumbiji wapo kileleni mwa Kundi G wakiwa na pointi 9 kila mmoja wakifuatiwa na Botswana, Guinea, na Uganda wenye pointi 6 kila mmoja huku Somalia ikiburuza mkia bila pointi yoyote
1. Utii. Mwanamke akikupenda atakutii katika mambo yote ambayo ni halali. Hii ni Ishara kuu. Tofauti na hapo Hakupendi. 2. Kuwasiliana Kila muda atakuwa anawasiliana na wewe. Haiwezi kupita siku bila kuwasiliana nawe. Tofauti na hapo Hakupendi. 3. Huacha Tabia Mbaya Anabadilisha tabia zake mbaya zinazokuudhi. Hawezi kurudia kosa moja kila siku. Tofauti na hapo hakupendi 4. Ana anza kukuiga. Kama unapenda jambo fulani nae ataanza kulipenda. Mf kama unapenda Timu ya Simba naye ataanza kuipenda. Tofauti na hapo Hakupendi. 5. Kuonana Nawe Siku zote atapata njia ya kukutana nawe hata iweje. Ukiona anakupa visingizio na visababu sijui nauli hana, jua hakupendi. 6. Anakuombea. Mwanamke anayekupenda atakuombea ili mambo yako yanyooke. Tofauti na hapo ujue hakupendi, akuombee ili iweje 7. Anakuonea Wivu. Anajisikia wivu akikuona upo au unachat na wanawake wengine. Hawezi kabisa na lazima akwambie. Tofauti na hapo Hakupendi. 8. Kukupa Zawadi. Sio kwamba Wanawake hawana pe...
Comments