- Get link
- Other Apps
Wasanii
wa sanaa za maigizo maarufu kama ‘Bongo Movies’ wanaoishabikia klabu ya
Simba leo wamekabidhiwa kadi za uanachama wa klabu hiyo yenye maskani
yake mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam ikiwa ni kuelekea kwenye
kilele cha siku ya Simba ijulikanayo kama ‘Simba Day’ ambayo
huadhimishwa kila ifikapo Agosti 8 kila mwaka.
Mwenyekiti
wa klabu hiyo Evans Aveva ndiye aliyewakabidhi kadi hizo wasanii
wakiongozwa na Jacob Steven ‘JB’, Mtitu, Monalisa pamoja na Odama ambao
wote kwa pamoja wakekuwa wanachama wapya wa klabu hiyo kuanzia sasa.
Baada
ya kukabidhiwa kadi zao JB alizungumza kwa niaba ya wenzake akisema
anajisikia fahari kubwa kukabidhiwa kadi ya uanachama wa Simba kwasabu
klabu hiyo ni moja kati ya timu kubwa barani Afrika yenye historia ya
aina yake katika soka la Tanzania na Afrika kwa ujumla na anafurahi kuwa
mmoja wa wanachama wa klabu hiyo.
“Simba
ni klabu kubwa iliyojaa historia ya aina yake na mimi najivunia kuwa
mwanachama wa klabu hii japo timu yetu imekuwa haifanyi vizuri sana kwa
siku za hivi karibuni”, amesema JB.
“Klabu
ya Simba imeanza kutambua mchango wa wasanii kwenye timu yao na ndio
imekuwa klabu ya kwanza nchini kukabidhi kadi kwa wasanii hadharani kama
hivi, lakini usishangae kuona vilabu vingine vimeiga na kufanya hiki
ambacho kimefanywa leo na klabu ya Simba”, aliongeza.
Katika
hatua nyingine, Simba imesema imeialika timu ya FC Leopards kuja
kucheza mchezo wa kirafiki katika kusherehekea siku ya Simba Day
itakayoadhimishwa Agosti 8 mwaka huu. Rais wa Simba Bw. Aveva ameongeza
kuwa, siku hiyo kutakuwa na mechi ya utangulizi kati ya viongozi wa
Simba watakao kipiga dhidi ya wasanii wa Bongo Movies kabla ya mtanange
wa Simba SC dhidi ya FC Leopard.
Comments