HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI
DK JAFO ATEUA WAJUMBE WA TUME YA USHINDANI FCC
TIDO MHANDO KUONGOZA BODI MPYA YA ITHIBATI YA WANAHABARI
MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMAAA...
𝗠𝗕𝗢𝗪𝗘 𝗔𝗦𝗜𝗧𝗜𝗦𝗛𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗗𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗬𝗔 𝗖𝗛𝗔𝗗𝗘𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗧𝗔𝗥𝗘𝗛𝗘 𝟮𝟯.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, ametangaza kusitishwa kwa maandamano yaliyokuwa yamepangwa kufanyika tarehe 23 Septemba 2024. Mbowe alitoa tangazo hilo kupitia mazungumzo ya moja kwa moja kwenye jukwaa la Space katika mtandao wa kijamii wa X (zamani ukijulikana kama Twitter). Mbowe alisema kuwa maamuzi haya yamefikiwa kwa kuzingatia hali ya sasa ya kisiasa na maslahi mapana ya taifa. Alieleza kuwa lengo la maandamano lilikuwa ni kuonesha hisia za wananchi na kudai haki na uwajibikaji wa serikali, lakini kwa sasa wameamua kutoa nafasi kwa mazungumzo na njia za amani kufanikisha malengo yao. Pia aliwahimiza wanachama na wafuasi wa CHADEMA kuendelea kuwa watulivu huku wakiangalia mwelekeo wa mazungumzo hayo na hatua nyingine za kisiasa.
MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMAAA....
MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMAAA...
KAMATI YA UWT KUTOA MSAADA WA KISHERIA NCHINI
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Haki na Sheria ya Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania (UWT), Zainab Katimba amesema kuwa UWT ina mpango wa kuanzisha Kanzi Data ya Mawakili Wanawake watakaokuwa wanatoa msaada wa kisheria nchini. Akielezea mikakati ya kamati hiyo, Katimba amesema wataweka utaratibu wa mawakili hao pamoja na washirika wao wa kutoa huduma ya msaada wa kisheria kila wiki ya mwisho ya mwezi katika mikoa mbalimbali nchini kwa lengo la kuwafikia walengwa zaidi. IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA MSIMAMIZI MKUU KAMANDA WA MATUKIO ONLINE TV 0754264203
Comments