MKE WA WAZIRI MKUU ATOA MSAADA WA MASHUKA KWA AKINAMAMA WALIOJIFUNGUA


1Waziri Mkuu, Kassim Majalaiwa akizungumza  na  Madaktari, Wauguzi na watumishi wa hospitali ya wilaya ya  Ruangwa  Aprili 11, 2016.  Kushoto ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na wapili kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wa mkoa Lindi, Mzee Mtopa.
2Mke  wa  Waziri Mkuu, Mary Majalaiwa akizungumza baada ya kukabidhi msaada wa shuka kwa wazazi wanaosubiri kujifungua na waliojifungua kwenye hospitali ya wilaya ya  Ruangwa  Aprili 11, 2016.  Kushoto ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na wapili kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wa mkoa Lindi, Mzee Mtopa.
5Wanawake  wa  Ruangwa wakimshangilia Waziri Mkuu,   Kassim Majaliwa wakti alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Chama cha Walimu mjini Ruangwa Aprili 11, 2016.
6Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akiagana na wanwake  wa Ruangwa  baada ya kuzungumza nao kwenye  ukumbi wa  Chama cha Walimu  mjini Ruangwa  Aprili  11, 2016.
3Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akitembelea soko  kuu la mji wa Ruangwa  kukagua hali ya chakula na bei zake Aprili  11, 2016. Alikuwa katika ziara ya jimbo lake la uchaguzi la Ruangwa.
4  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na  mabingwa wa soka wa mkoa wa Lindi , timu ya   Namungo FC ya Ruangwa baada ya kukabidhiwa kombe  la ubingwa huo na kuzungumza nao kwenye uwanja wa michezo wa Ruangwa akiwa katika ziara jimboni kwake , Aprili 11, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri  Mkuu)
…………………………………………………………………………………………………….
MKE wa Waziri Mkuu, Mary Majaliwa amefanya ziara katika Hospitali ya wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi na kutoa msaada wa mashuka kwa akinamama waliojifungua.
Pia ametumia fursa hiyo kuwapongeza madaktari na wauguzi wa Hospitali ya wilaya ya Ruangwa kutokana na kuwahudumia vizuri wananchi na kuwaomba  waendelee kufanya kazi hiyo kwa mujibu wa maadili ya kazi yao.
Mke wa Waziri Mkuu ameyasema hayo jana  wakati alipotembelea wodi ya akinamama waliotoka kujifungua na kufurahishwa na hali ya utoaji huduma hospitalini hapo, ambapo  aliwasisitiza kuendelea moyo huo kwa sababu wao ndio wamebeba dhamana ya afya za wananchi.
“Nimefurahi kukuta wazazi wanahudumiwa vizuri na wenyewe wamekiri kwamba huduma zinazotolewa hospitalini hapa ni za kuridhisha, tofauti na tulivyozoea kusikia wagonjwa wakiwalalamikia wauguzi, hivyo ni jambo la kujivunia, hongereni sana” amesema.
Mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika wodi hiyo Hamisa Rashid ambaye amelazwa katika wodi hiyo  amesema alifikishwa hospitalini hapo wiki mbili zilizopita akiwa katika hali mbaya na ameweza kuhudumiwa vizuri na sasa anakaribia kutoka.
“Mimi nilikuwa sijitambui, siwezi kufanya kitu chochote lakini baada ya kuletwa hospitalini hapa madaktari kwa kushirikiana na wauguzi wamenihudumia vizuri na sasa naweza hata kwenda chooni mwenyewe na bila msaada wao mimi ningekuwa nimepoteza maisha kutokana na hali yangu ilivyokuwa,” amesema Hamisa.
Mbali na kutoa msaada huo wa mashuka pia ametoa baiskeli mbili kwa ajili ya wanawake wawili walemavu lengo likiwa ni kuwawezesha kufanya shughuli zao za kijamii kwa urahisi.
Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Rehema Omary amemshukuru mke wa Waziri Mkuu kwa msaada huo, ambapo alimuomba Waziri Mkuu, Majaliwa awawezeshe kwenda kushiriki katika shughuli mbalimbali zinazofanywa na walemavu ikiwemo michezo.
Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi amewataka watumishi wa hospitali hiyo kufanya kazi kwa bidii na kuachana na utendaji kazi wa mazoea kwa sababu umepitwa na wakati.
Pia amesema amefurahishwa  na kitendo cha wagonjwa kukiri kuwa wanahudumiwa vizuri tofauti na hospitali zingine hivyo kuwataka kuendelea na ari hiyo ya kufanya kazi kwa bidii, maarifa na weledi mkubwa.
Imetolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MUSTAFA MKULO AFARIKI DUNIA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

MAKALLA ASHANGILIWA BUNGENI

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI

BASHASHA LATAWALA NCHIMBI ALIPOLAKIWA NA CHONGOLO SONGWE

NCHIMBI AFUNGUA KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA KUMBUKIZI YA MWALIMU NYERERE

DKT NCHIMBI AKARIBISHWA KIMILA NYUMBANI RUVUMA