SAMATTA APEWA JEZI NAMBA 10 GENK


Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta kuanzia msimu ujao atakuwa anavaa jezi namba 10 badala ya 77 katika klabu yake, KRC Genk ya Ubelgiji.
Kupitia akaunti yake ya Instagram, Genk imeandika; “Mbwana Samatta msimu ujao atachezea (jezi) namba 10,”.
Na hiyo ndiyo jezi ambayo Samatta anaivaa hadi katika timu yake ya taifa, Taifa Stars ambayo yeye ni Nahodha. 
Lakini aliposajiliwa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), klabu yake ya mwisho ya Afrika kuchezea, Samatta alianza kwa kuvaa jezi namba 15 kabla ya baadaye kupewa namba 9.
Baada ya msimu mmoja na nusu, Samatta amecheza mechi 60 Genk na kufunga mabao 20 tangu amejiunga nayo Januari mwaka jana akitokea TP Mazembe ya DRC, kati ya hizo mechi 18 alicheza msimu uliopita na 42 msimu huu na kati ya hiyo, ni michezo 38 tu ndiyo alianza, 10 msimu uliopita na 28 msimu huu.
Mechi 21 kati ya hizo alitokea benchi, nane msimu uliopita na 13 msimu huu, wakati 11 hakumaliza baada ya kutolewa, tano msimu uliopita na sita msimu huu na katika mabao yake 20, 15 amefunga msimu huu na matano msimu uliopita.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MUSTAFA MKULO AFARIKI DUNIA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

MAKALLA ASHANGILIWA BUNGENI

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI

BASHASHA LATAWALA NCHIMBI ALIPOLAKIWA NA CHONGOLO SONGWE

NCHIMBI AFUNGUA KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA KUMBUKIZI YA MWALIMU NYERERE

DKT NCHIMBI AKARIBISHWA KIMILA NYUMBANI RUVUMA