Mkurugenzi Mtendaji
wa Taasisi ya Hope For All , Edger Mwamfupe akipata chakula cha mchana wanafunzi wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa
kujitambua wanafunzi waliomaliza Kidato cha Nne katika Shule ya Sekondari ya
Makongo Juu, Dar es Salaam hivi karibuni.
Na Richard Mwaikenda-Dar
Wanafunzi wakisikiliza kwa makini wakati wa mafunzo hayo
Mkuu wa Kitengo cha Vijana cha Taasisi hiyo, Harrison Edger akiwa tia moyo wanafunzi hao
aitwaye Davis Eugene ambaye ndoto yake ni kuwa Rais wa Nchi.
Wanafunzi wakimsikiliza kwa makini Meneja Utawala wa Taasisi hiyo, Fides Uisso alipokuwa akiwaeleza jinsi ya kuwa na uthubutu wa kutimiza ndoto zao
Wanafunzi wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Kitengo cha Vijana, Harrison alipokuwa akifundisha jinsi ya kujiandaa kimaisha kwa kuanzisha miradi mbalmbali ya maendeleo.
Fides Uisso akibadilishana mawazo na wanafunzi kwenye viwanja vya shule hiyo
Na Richard Mwaikenda-Dar
WANAFUNZI waliomaliza Kidato cha Nne, wametakiwa kuachana na tabia ya kupoteza
muda kusubiri kurithi mali za wazazi wao,
bali wajitambue kwa kufanya kazi kwa
bidii kujiletea maendeleo.
Kauli hiyo ilitolewa
na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya
Hope For All , Edger Mwamfupe wakati wa
mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kujitambua wanafunzi waliomaliza Kidato cha Nne
katika Shule ya Sekondari ya Makongo Juu, Dar es Salaam hivi karibuni.
“Kila mmoja ajitambue kivyake,, simama wewe kama wewe,
jitambue wewe ni nani, ukijiami kama unaweza na utaweza kweli. Mkome kutegemea
kurithi mali za baba zenu,” aliwaaasa Mwamfupe.
“Msiruhusu ndoto zenu zife, hata kama mtakumbana na mazingira magumu majumbani
kwenu, mzishikile msiruhusu ndoto zenu zife, Kawaida wewe ndiyo unaamua kuwa
tajiri au masikini , utajiri uko kichwani kwako,” alisisitiza Mwamfupe huku
akipigiwa makofi na wanafunzi.
Mwamfupe, hakusita
kujitolea mfano yeye kuhusu maisha yake ya ujana, ambapo aliwaeleza kuwa licha
ya utajiri wa babake, lakini yeye aliamua kujitegemea tangu akiwa anasoma na
kwamba alipokuwa ana miaka 19 alinunua gari aina ya Toyota Corola (Mayai).
Pia, kupitia kipaji
chake cha kucheza mpira na ngoma za asili kilifanya kwa mara ya kwanza apande
ndege kwenda Romania kuiiwakilisha Taifa
katika Tamasha la Ngoma.
Pia aliwahi miliki bendi ya Muziki wa dansi.Mkuu wa Kitengo cha Vijana cha Taasisi hiyo, Harrison Edger
aliwataka vijana wenzie wanapoingia
mitaani ambako kuna mambo mengi mazuri
na mabaya , inatakiwa wajiwekee mipango
yao ya maendeleo ya muda mfupi na muda mrefu.
“Mungu alituumba watu wote tukiwa na bongo moja, hakuna
mwenye bongo mbili, hivyo hata wewe
unaweza, ondoa hofu utashinda. Fanyeni
mambo yenu mazuri mapema ili baadaye mkizeeka mje muishi vizuri.”
Naye Mkuu wa Kitengo cha Wanawake na Watoto wa Taasisi hiyo,
Juliana Mushi aliwaasa watoto wa kike kuacha tabia ya kujihusisha na umalaya
ili waje kuwa wazazi wazuri wa baadaye.
Aliwataka badala ya kujihusisha na mambo hayo mabaya bali wawe
wanajishughulisha na mambo ya uzalishaji
mali, ikiwemo ujasiriamali.
Wakati wa mafunzo hayo wanafunzi walipata wasaa wa kila
mmoja kuelezea kuwa ndoto yake ya maisha atakuwa nani. Baadhi wanataka kuwa
wajasiriamali, madaktari, mawaziri, walimu, wakandarasi, wasanii maarufu,
waandishi wa habari na mmoja
aitwaye Davis Eugene yeye alitaka awe
Rais wa Nchi.
Taasisi hiyo ina mpango wa kuanzisha Klabu za mafunzo kama
hayo katika shule mbalimbali nchini na kwa Dar es Salaam wameanza kuweka klabu
katika shule hiyo ya Makongo Juu. Lengo ni kuwataka wanafunzi waliomaliza elimu
hiyo kuwa na kazi ya kufanya wanaposubiri matokeo ya kujiunga kidato cha tano
na wanaoshindwa kujiunga waendeleze ndoto zao.
Mkurugenzi Mtendaji
wa Taasisi ya Hope For All , Edger Mwamfupe (Kulia), akimsikiliza mmoja wa wanafunzi aliyekuwa akijieleza jinsi atakavyokabiliana na maisha baada ya kumaliza shule..Wanafunzi wakisikiliza kwa makini wakati wa mafunzo hayo
Mkuu wa Kitengo cha Vijana cha Taasisi hiyo, Harrison Edger akiwa tia moyo wanafunzi hao
aitwaye Davis Eugene ambaye ndoto yake ni kuwa Rais wa Nchi.
Wanafunzi wakimsikiliza kwa makini Meneja Utawala wa Taasisi hiyo, Fides Uisso alipokuwa akiwaeleza jinsi ya kuwa na uthubutu wa kutimiza ndoto zao
Wanafunzi wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Kitengo cha Vijana, Harrison alipokuwa akifundisha jinsi ya kujiandaa kimaisha kwa kuanzisha miradi mbalmbali ya maendeleo.
Fides Uisso akibadilishana mawazo na wanafunzi kwenye viwanja vya shule hiyo
Comments