GAVU AHIMIZA WANACHAMA CCM KULIPIA ADA WAWE HAI


Katibu wa Nec Oganaizesheni  wa Chama cha Mapinduzi Issa haji Gavu amewataka wanachama wa CCM kuhudhuria vikao sambamba na kulipia kadi ili waendelee kuwa wanachama hai. 


Gavu amesema hayo Mei 29,2023 alipokuwa akizungumza na wananchi baada ya kushiriki Mkutano Kwa Balozi wa Shina Na. 04  Kata ya Ifunda katika halmashauri ya wilaya ya Iringa akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa CCM ambaye yupo mkoani Iringa kwa ziara ya siku 7 ya kukagua uhai wa chama na utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM. 


Amesema kuwa wanachama hai itasaidia CCM kuendelea kuwa chenye mvuto na oitaendelea kuaminiwa na kuthaminiwa na watanzania huku akisema hakuna chama chenye mvuto kwa wananchi  kama  CCM.


Katika hatua nyingine GAVU amesema Tanzania ni nchi yenye demokrasia ndio maana kumekuwa na majadiliano sambamba na kumpa Uhuru kila mtanzania kutoa maoni.



Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

UKWELI KUHUSU TENDO LA NDOA NA FAIDA ZAKE

HUYU NDIYE WANU HAFIDH, CHAMPIONI WA ELIMU

MAWAZIRI WALIOACHWA HAWA HAPA

๐Œ๐‰๐”๐„ ๐Š๐€๐‚๐‡๐„๐‘๐Ž ๐Œ๐™๐„๐๐€

HISTORIA YA MAREHEMU MC PILIPILI

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

USIKUBALI KUWA LOFA KWA MWANAMKE...

NAPE AWAPA UKWELI VIJANA