Wachezaji wa timu za mchezo wa Pete za watumishi na wanafunzi wa Chuo Cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), wakichuana wakati wa bonanza la michezo la kujenga uhusiano baina ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbongwe na Chuo hicho.
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
Bonanza hilo ambalo ngeni rasmi alikuwa Mkuu wa Chuo hicho, Profess Hozen Mayaya lilishuhudiwa pia na Mbunge wa Jimbo la Mbogwe, Nicodemus Maganga limefanyika leo Juni 3, 2023 katika viwanja vya Shule ya John Merlin jijini Dodoma.
Michezo iliyoshindaniwa ni soka, Pete, mbio, kuvuta kamba, mbio za magunia na mchezo wa kufukuza kuku.
Kwa upande wa soka timu za Mbogwe na Mipango zilitoka sare ya mabao 2-2, mbio walishinda Mbogwe, kuvuta kamba walishinda Mipango, mbio za magunia Mbogwe, kufukuza kuku walishinda Mipango na Pete ushindi ulienda kwa watumishi wa Mipango kwa vikapu 18-15.
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
Comments