EWURA YAHAMASISHA WADAU KUPELEKA HUDUMA YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA VIJIJINI KAHAMA

 MENEJA EWURA Kanda ya Magharibi, Mhandisi. Walter Christopher, amewahamasisha wamiliki wa vituo vya mafuta kupeleka huduma ya nishati safi ya kupikia vijijini ili kuunga mkono jitihada za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Mhandisi Christopher ametoa wito huo wakati wa mafunzo ya siku moja kwa wadau wa mafuta Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga .

Mhandisi Christopher amesema kuwa Serikali inaendelea kuhamasisha wananchi kutumia Nishati Safi ya kupikia ili kulinda afya, kuokoa gharama na muda sambamba na kulinda Mazingira.

“Nishati Safi ya kupikia ina manufaa makubwa kwetu binadamu na mazingira kwa ujumla hivyo nawaomba wamiliki wa vituo vya mafuta muunge mkono jitihada za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za  kupeleka huduma hiyo  kwa wananchi wa vijijini ili waweze kutumia nishati safi ya kupikia.”amesema Mhandisi Christopher

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TAPSOA Wilaya ya Kahama, Bw. Alley Abeid Salum ameishukuru EWURA kwa elimu na anaamini kuwa itatoa majibu ya changamoto zinazowakabili wadau wa mafuta.



Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

UKWELI KUHUSU TENDO LA NDOA NA FAIDA ZAKE

HUYU NDIYE WANU HAFIDH, CHAMPIONI WA ELIMU

MAWAZIRI WALIOACHWA HAWA HAPA

๐Œ๐‰๐”๐„ ๐Š๐€๐‚๐‡๐„๐‘๐Ž ๐Œ๐™๐„๐๐€

HISTORIA YA MAREHEMU MC PILIPILI

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

USIKUBALI KUWA LOFA KWA MWANAMKE...

NAPE AWAPA UKWELI VIJANA