"Naifahamu Yanga, sio Timu ngeni kwangu, ni moja ya Klabu za kisasa Ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara.. Siku wanacheza Fainali ya #CAFCC nilikuwepo uwanjani kama Ofisa wa CAF TV na nilipewa nafasi ya kufanya mazungumzo ya Karibu na Kocha wao wa Wakati huo Nasserdin Nabi na wachezaji kadhaa.. walicheza mchezo mzuri na asilimia kubwa ya wachezaji waliokuwa nao kipindi kile naona wanao mpaka sasa"
"Naamini Yanga watakuwa ni changamoto nzuri zaidi kwetu katika mashindano haya msimu huu na mechi yetu ijayo dhidi yao ni ya kuoneshana ubora wa Timu hizi mbili pande zote."
Maneno ya Kocha Mkuu wa MC Algers, Patrick Beaumelle jana baada ya mchezo wa League 1 dhidi ya Entente Sportive Setifienn

Comments